Mkurugenzi
wa Taasisi ya Nitetee Foundation ya Jijini Mwanza, Flora Lauwo asubuhi
ya leo Machi 23, 2019 amepokelewa kwa shangwe katika uwanja wa ndege wa
Mwanza akitokea nchini Oman alikokuwa amealikwa kutokana na mchango wake
mkubwa wa kusaidia watu mbalimbali wenye uhitaji katika jamii kupitia
taasisi yake.
Mwezi mmoja uliopita, Lauwo kupitia Ubalozi wa Tanzania alialikwa nchini Oman ambapo Machi 08, 2019 kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani alipatiwa tuzo mbili za kama ishara ya kutambua mchango wake wa kuwasaidia wenye uhitaji katika jamii.
Pia kwenye maadhimisho hayo (Siku ya Wanawake Duniani 2019), Lauwo alipewa tuzo kupitia tamasha la Binti Filamu lililofanyika Jijini Mwanza na hivyo kufanya idadi ya tuzo alizopokea mwaka huu kuwa tatu. Lauwo pia amewahi kushinda tuzo ya Malikia wa Nguvu inayotolewa na Clouds Media Group.
Mwezi mmoja uliopita, Lauwo kupitia Ubalozi wa Tanzania alialikwa nchini Oman ambapo Machi 08, 2019 kwenye Maadhimisho ya Siku ya Wanawake Duniani alipatiwa tuzo mbili za kama ishara ya kutambua mchango wake wa kuwasaidia wenye uhitaji katika jamii.
Pia kwenye maadhimisho hayo (Siku ya Wanawake Duniani 2019), Lauwo alipewa tuzo kupitia tamasha la Binti Filamu lililofanyika Jijini Mwanza na hivyo kufanya idadi ya tuzo alizopokea mwaka huu kuwa tatu. Lauwo pia amewahi kushinda tuzo ya Malikia wa Nguvu inayotolewa na Clouds Media Group.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...