Mkuu wa Mkoa wa Dar es Salaam Mhe. Paul Makonda akiwa na Rais wa Tanzania Basketball Federation (TBF) Phares Magesa, mara baada ya mazungumzo kuhusu maendeleo ya mpira wa Kikapu ambapo pia walipeana mrejesho kuhusu utekelezaji wa mradi wa ujenzi wa uwanja wa ndani wa kikapu katika mkoa wa Dar es Salaam, ujenzi wa uwanja wa ndani wa Kikapu na michezo mingine utaanza karibuni mara baada ya mazungumzo na wafadhili wa mradi kukamilika, TBF inamshukuru Mhe. 

Makonda kwa ushirikiano wake katika kuhakikisha mkoa wa Dar es Salaam unapata viwanja vya kisasa vya Kikapu na Michezo mingine na Shirikisho linaomba Wakuu wa Mikoa, viongozi wa ngazi mbalimbali na wadau wa maendeleo waige mfano wa Mhe. Makonda na Mhe. Anthony Mtaka katika kutatua changamoto ya miundombinu ya michezo nchini Tanzania, pia TBF inamshukuru sana Rais wa Tanzania Mhe. Dkt. John Magufuli kwa kuwawezesha Makao Makuu Dodoma kupata mradi wa ujenzi wa uwanja wa kisasa wa michezo ambao nao utaanza karibuni kwa ufadhili wa Mfalme wa Morocco, www.tbf.or.tz

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...