Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa Sportpesa, Tarimba Abbas 
Klabu ya Soka ya Simba yenye maskani yake Msimbazi jijini Dar es Salaam imepongezwa na Kampuni yakubashiri nchini ya SporPesa baada yakufanya vyema kwa kufuzu Robo Fainali ya Michuano ya Ligi ya Mabingwa barani Afrika. 

Simba SC kupitia ukurasa wake rasmi wa Instagram, imethibitisha kuwa SportPesa kutoa kiasi cha pesa cha 50,000,000/= kama pongezi baada yakutinga hatua ya Robo Fainali ya Michuano hiyo mikubwa barani Afrika kwa ngazi ya klabu.

Taarifa hiyo imesema: "Mkurugenzi wa Utawala na Udhibiti wa Sportpesa, Tarimba Abbas ameipongeza timu hiyo kutinga hatua ya Robo Fainali ya Michuano ya CAF ambapo amethibitishwa kuwa Kampuni hiyo itakabidhi kiasi cha Tsh 50,000,000/= kama zawadi Kimkataba".

Simba SC  ilifuzu hatua hiyo baada yakuifunga AS Vita lub bao 2-1 kwenye dimba la Uwanja wa taifa jijini Dar es Salaam, hata hivyo Mnyama atasubiri droo ya Robo Fainali ya Michuano hiyo itakayopangwa majira ya Saa 2 Usiku, nchini Misri kujua anakabitiana na nani katika Robo Fainali.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...