Na Woinde Shizza,Arusha
Naibu waziri wa viwanda,baishara na uwekezaji mhandisi Stela Manyanya ameitaka taasisi ya  uhandisi na usanifu wa mitambo Tanzania(temdo )kuendelea kuwa  wabunifu  zaidi  katika uzalishaji wao  wa teknolojia ili  wawweze kusanifu mitambo inayokidhi malengo ya serikali  ya kuanzisha taasisi hiyo.
Injinia manyanya aliyasema hayo wakati kamati  ya  bunge  ya viwanda,biashara na mazingira ilipotembelea taasisi ya TEMDO kwa lengo la kukagua utekelezaji wa miradi.
Amesema kwa kuwa serikali inatambua mchango mkubwa wa Temdo katika kusanifu mitambo ni vema tasisi hiyo ikaongeza ubunifu zaidi katika uzalishaji ili kukidhi mahitaji ya serikali ya kuzalisha bidhaa zinazoenda na wakati
Ameongeza kuwa serikali itaangalia namna ya kuendelea kuziwezesha taasisi hizo za utengenezaji wa zana za kilomo na mashine   kwa kuzitolea fedha za bajeti ili ziendelee kuzalisha zana na mitambo yenye kukidhi mahitaji ya wananchi na viwanda.
Kwa upande wake Mwenyekiti Wa kamati yakudunu ya bunge viwanda ,biashara na Mazingira aliwataka pia taasisi hiyo kujiendesha kibiashara  zaidi ,wazalishe fedha za ndani.
"Nendi kibiashara zaidi mtazalisha fedha zenu wenyewe ambazo zitawasaidia kuendelea kujiendesha hata kama fedha za bajeti za serikalini zikichelewa kuwafikia nyie mnaendelea kujiendesha wenyewe sio kukaa na kusubiri tu fedha za bajeti zije" alisema Mwenyekiti.
Kaimu meneja wa ushauri viwandani   kutoka taasisi ya TEMDO Alexander Komba   amesema ujio wa kamati ya bunge katika tassisi hiyo kunaiwezesha serikali kuweza kuongeza nguvu zaidi iliwaweze kuwa wabunifu  katika  teknolojia zenye kukidhi mahitaji ya soko kufuatia vitendea kazi wanavyonunua kupitia fedha wanazopewa za bajeti.
Kamati ya Kudumu  Bunge  ya viwanda ,biashara na mazingira ikikagua mashine zilizopo katika taasisi ya uhandisi na usanifu mitambo Tanzania (TEMDO) iliopo jijini Arusha (Picha na Woinde Shizza).


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...