Baadhi ya wafanyabiashara ya matunda katika Jiji la Dar es Salaam wakiendelea na biashara zao ambapo wameimbia Michuzi Blog kuwa wanamshukuru Rais Dk.John Magufuli kwa uamuzi wake wa kutaka wafanyabiashara ndogondogo kuwa na vitambulisho na kutamulika rasmi.
Wafanyabiashara hao walieleza kuwa kwa sasa wanaheshimika na usumbufu waliokuwa wakiupata hapo awali kabla ya kuwa na vitambulisho haupo,"kwakweli utulivu wa biashara zetu umesaidia hata kuongeza wateja kwani yale mambo ya kukimbiakimbia yamekwisha,hivyo kwa hakika tunamshukuru Rais Magufuli na Serikali yake ya Awamu ya Tano kwa namna ambavyo imekuwa ikiwajali wanyonge",alisema Fredi Nyasiki mkazi wa Kimara ambaye hufanya biashara zake za matunda katikati ya jiji la Dar.
Wafanyabiashara wa matunda mbalimbali wanaotumia baiskeli wakiwahudumia wateja, kama walivyokutwa na Kamera ya Michuzi blog kando ya Barabara ya Samora, Dar es Salaam leo,vijana wengi kwa sasa wana vitambulisho vya wajasiliamali almaarifu kwa jina la vitambulisho vya Wamachinga vilivyotolewa na Rais Dkt John Magufuli hivi karibu kwa Wakuu wa mikoa yote nchini . (Picha na Emmanuel Massaka,MMG)
wafanyabiashara wakiendelea kukatiza katika viunga vya Jiji la Dar es Salaam.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...