Mkuu wa mauzo wa Vodacom Tanzania Kanda ya Kaskazini, Brigita Stephen (kulia) akimkabidhi zawadi Mkuu wa shule ya sekondari Arusha Day, Joyce Gyunah katika hafla iliyofanyika jijini Arusha jana. Katika kuadhimisha wiki ya wanawake duniani, Wafanyakazi wa Vodacom wametembelea shule hiyo ya wasichana na kuwapatia vifaa kwa ajili ya mahitaji yao ya shule ikiwa ni jitihada za kuhakikisha watoto wa kike wanafanya vizuri katika masomo na wanatimiza ndoto na malengo yao.

Mkuu wa mauzo wa Vodacom Tanzania Kanda ya Kaskazini, Brigita Stephen akizungumza na wanafunzi wa kike wa shule ya sekondari Arusha Day na kuwahimiza kusoma kwa bidii, katika hafla iliyofanyika jijini Arusha jana. Katika kuadhimisha wiki ya wanawake duniani, kampuni ya Vodacom imetembelea shule hiyo ya wasichana na kuwapatia vifaa kwa ajili ya mahitaji yao ya shule ikiwa ni jitihada za kuhakikisha watoto wa kike wanafanya vizuri katika masomo na wanatimiza ndoto na malengo yao.

Meneja Masoko wa kampuni ya Vodacom Tanzania kanda ya Nyanda za juu kusini, Magreth Lawrence (kushoto) akimkabidhi daftari, Jackline Chaula, mwanafunzi wa kidato cha tano katika shule ya sekondari ya Sangu jijini Mbeya. Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani, wafanyakazi wa kampuni hiyo wametembelea, kuongea na kutoa zawadi na vifaa mbalimbali kwa wasichana ili kuwasaidia mahitaji yao ya shule ikiwa ni jitihada za kuhakikisha watoto wa kike wanafanya vizuri katika masomo na wanatimiza ndoto na malengo yao.
Meneja Masoko wa kampuni ya Vodacom Tanzania kanda ya Nyanda za juu kusini, Magreth Lawrence, akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Sangu juu ya umuhimu wa elimu kwa watoto wa kike. Katika kuadhimisha siku ya wanawake duniani, wafanyakazi wa Vodacom Tanzania wametembelea shule hiyo na kuwapatia vifaa mbalimbali kwa ajili ya mahitaji yao ya shule ikiwa ni jitihada za kuhakikisha watoto wa kike wanafanya vizuri katika masomo na wanatimiza ndoto na malengo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...