Mkuu wa Wilaya ya Arumeru,Jerry Muro amehimiza uchangiaji wa ujenzi wa majengo ya taasisi za dini na kuacha kutegemea wahisani ambao wamekuwa na masharti magumu.

Muro ametoa rai hiyo alipokuwa mgeni rasmi katika hafla ya kuchangia ujenzi wa msikiti Mdogo wa Kati uliopo Ngarenaro unaogharimu kiasi cha zaidi ya milioni 800.

Amesema ipo Haja kwa waumini kuimarisha juhudi zao wenyewe katika uchangiaji jambo ambalo litafanikisha kukamilisha ujenzi kuliko kutegemea michango ya wahisani ambayo imekuwa haifiki kwa wakati.

Muro ambaye amekubali kuwa mwanakamati wa ujenzi wa msikiti huo, ametoa kiasi cha sh,milioni 1,huku akiahidi kutoa fulana 100 kwa ajili ya kuhamasisha uchangiaji na ameahidi kumsomesha hadi chuo kikuu mtoto wa miaka 7, Abdulkarim Hasan baada ya kuvutiwa na uwezo wake mkubwa katika kuielewa wa dini ya kiislam.

Awali imamu wa msikiti huo,Hasan Kileo,amesema ujenzi wa msikiti huo utasaidia kuingiza idadi kubwa ya waumini tofauti na ule wanaosalia kwa sasa na utagharimu kiasi cha sh,milioni 800 nakwamba hadi sasa wamefanikiwa kupata sh,milioni 18 ambayo imetumika katika ujenzi wa msingi.

Naye sheikh Haruna Husen pamoja na kumshukuru mgeni rasm Jeri Muro kwa kuchangia ujenzi huo wa msikiti lakini aliwataka waumini wa kiislamu kuwa mstari wa mbele kujitoa katika ujenzi wa nyumba za Mungu.
Aliwataka waumini kujivunia kila walichokijenga wao kuliko kujengewa na mtu mwingine .pamoja na harambee hiyo watoto zaidia ya 50 wamehitimu elimu ya madrasa na kutakiw kufuata mema waliofundishwa
 Mkuu wa Wilaya ya Arumeru,Jerry Muro akiwa ameketi katikati ya watoto wa madrasa wakimsomea  huku wakimsomea dua. 
 Wanafunzi waliomaliza madrasa wakiwa wanasikiliza kwa makini hutuba ya mkuu wa wilaya
 Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akiwa anahutubia katika harambee ya kuchangia msikiti wa  Ngarenaro uliopo jijini Arusha

 picha ikionyesha wa kwanza kushoto sheikh Haruna Husen akifuatiwa na mkuu wa wilaya ya Arumeru  Jerry Muro wa tatu ni imamu wa msikiti wa Ngarenaro ,Hasan Kileo, wakiwa wanafatilia harambee hiyo.
Mkuu wa wilaya ya Arumeru Jerry Muro akiwa na mtoto Abdulkarim Hassan ,ambapo mkuu wa wilaya amejitolea kumsomesha mtoto huyu 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...