Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Mheshimiwa Dkt. Damas Daniel Ndumbaro (Mb.), amefanya mazungumzo na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) nchini, Bw.Naofumi Yamamura, hivi karibuni katika ofisi za wizara Dodoma. Mazungumzo hayo, yanalenga kuimarisha ushirikiano wa Tanzania na Japan kupitia shirika hilo katika masuala ya miundombinu. 
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro, akisalimiana na Mwakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) nchini, Bw. Naofumi Yamamura,mara baada ya kuwasili katika ofisi za wizara.
Afisa Mambo ya Nje wa Idara ya Asia na Australasia katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashiriki, Bi. Bertha Makilagi na Katibu wa Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Bw. Charles Faini, wakifuatilia mazungumzo hayo. 
Afisa Mwandamizi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA), Takusaburo Kimura, akifafanua jambo wakati wa mazungumzo hayo. 
Wawakilishi wa Shirika la Maendeleo la Kimataifa la Japan (JICA) nchini, Bw. Naofumi Yamamura na Afisa Mwandamizi wa shirika hilo, Bw. Takusaburo Kimura, wakimsikiliza Naibu Waziri wa mambo ya Nje na Ushirkiano wa Afrika Mashariki, Dkt. Damas Daniel Ndumbaro (hayupo pichani).

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...