GAVANA
wa Benki Kuu ya Tanzania (BoT), Prof. Florens Luoga, amesema elimu
kuhusu masuala ya fedha ni muhimu katika mfumo mzima wa taarifa za
mikopo ili kuwawezesha Watanzania kupanga matumizi bora ya mikopo.
Prof
Luoga alitoa kauli hiyo katika uzinduzi wa kampeni ya uelimishaji umma
kuhusu taarifa za mikopo na fedha iliyoratibiwa na BOT kwa kushirikiana
na taasisi ya International Finance Corporation ambayo ni mwanachama wa
Kundi la Benki ya Dunia.
Akizungumza
kwa niaba ya Waziri wa Fedha na Mpango, Dk. Philip Mpango, Prof Luoga
alisema taarifa za mikopo na elimu ya fedha ni muhimu ili kuhakikisha
Watanzania wanaondokana na matumizi ya anasa ya mikopo.
“Kampeni
hii ya elimu kwa umma inalenga kuwaelimisha watumiaji wa huduma za
fedha na wadau wengine kukuza uelewa wao kuhusu taarifa za mikopo ili
kuongeza ushiriki katika matumizi ya taarifa za mikopo hapa nchini,”
alisema.
Aidha,
Meneja Msaidizi, Mfumo wa Kumbukumbu za Wakopaji kutoka BoT, Nkanwa
Magina alisema kampeni hiyo ya miezi mitatu inalenga kuongeza uelewa,
mwamko kuhusu taarifa za mikopo na kukuza upatikanaji wa mikopo.
”Kauli
mbiu katika kampeni hiyo ni: “Pata Taarifa Yako ya Mikopo Leo. Angalia
hali yako ya kifedha ili kupanga mustakabali wako bora wa kesho”
inaungwa mkono na wadau mbalimbali katika sekta ya huduma za fedha.
“Wadau
hao wameahidi kusaidia kusambaza ujumbe kuhusu umuhimu wa upatikanaji
wa mikopo na jinsi Watanzania wanavyoweza kuishi maisha bora kwa kuweza
kupata taarifa za mikopo yao na kujua historia ya mikopo yao,” alisema.
Alisema usimamizi mzuri wa mikopo na historia nzuri ya mikopo ni muhimu katika kuwezesha kupata mkopo nafuu."Kuhakiki
taarifa yako ya mikopo mara moja kwa mwaka ni huduma inayopatikana bila
malipo, tena itakuletea mafanikio kwa kukuandaa vema utakapoenda kuomba
mkopo.
"Historia
nzuri ya mikopo inaweza kusaidia kustahili viwango vya chini vya riba
na ada, hivyo kuondokana na kutenga fedha kwa ajili ya dharura na
gharama zisizotarajiwa," alisema.
Alisema
mikopo inasaidia kupata mahitaji ya sasa, kama vile nyumba au ada ya
shule ya mtoto wako, kwa kuzingatia ahadi yako ya kulipa kwa awamu na
kwa muda uliopangwa.Aidha,
Meneja wa IFC - Tanzania, Manuel Moses alisema taarifa ya mikopo
inaonesha taarifa binafsi; utambulisho na taarifa ya mawasiliano na
ikiwezekana historia ya ajira; idadi na aina za akaunti za mikopo.
Naye
Meneja Maendeleo ya Biashara kutoka Dun & Bradstreet, Josephine
Temu alisema kwa sasa, kuna taasisi mbili zilizopatiwa leseni na Benki
Kuu ya Tanzania kuandaa na kutoa taarifa za mikopo hapa Tanzania ambazo
ni Creditinfo Tanzania Limited na Dun & Bradstreet.Alisema
taasisi hizo zinakusanya na kutunza taarifa za mikopo na kutoa taarifa
za mikopo kwa kampuni au watu wanaozihitaji kama vile benki.
Alisema
ripoti hiyo ya mikopo inaweza kutolewa na taasisi hizo (Creditinfo na
Dun & Bradstreet) mara moja kwa mwaka bila malipo.“Ili
kupata taarifa ya mikopo unatakiwa kuwasilisha nakala ya kitambulisho
chako cha taifa au kingine kama leseni ya udereva, hati ya kusafiria.
Jaza na wasilisha fomu ya maombi ya taarifa yako ya mikopo katika
taasisi zinazoandaa taarifa za mikopo ambazo kwa sasa ni Creditinfo au
Dun & Bradstreet," alisema.
Akifafanua
kuhusu mambo muhimu ya kuangalia kwenye taarifa ya mikopo, Meneja
Maendeleo ya Biashara kutoka Creditinfo, Tonny Missokia alisema muhimu
ni taarifa binafsi kama vile jina, hadhi ya ndoa, anwani, taarifa za
ajira na namba za mawasiliano ni sahihi.
Meneja
Msaidizi, Mfumo wa Kumbukumbu za Wakopaji kutoka BoT, Nkanwa Magina
akizungumza katika warsha ya kuhusu elimu ya taarifa za fedha na ripoti
za mikopo kwa wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma.
Meneja
Msaidizi, Mfumo wa Kumbukumbu za Wakopaji kutoka BoT, Nkanwa Magina
akizungumza katika warsha ya kuhusu elimu ya taarifa za fedha na ripoti
za mikopo kwa wanafunzi wa Chuo kikuu cha Dodoma.
Wataalam
wa Benki Kuu ya Tanzania, Creditinfo na Dun & Bradsheet wakitoa
elimu kuhusu umuhimu wa taarifa za mikopo kwa mwananchi eneo la Nyerere
Square mchana huu. Kampeni hiyo inaendeshwa kwa pamoja na Benki Kuu
ikishirikiana na International Finance Corporation ambayo ni sehemu ya
kundi la Benki ya Dunia
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...