Simu ya Tshs. 820,000 kuuzwa kwa Tshs. 8,000 tu!!!!!

Wateja kupelekewa bidhaa bure wakifanya manunuzi yatayaozidi Tshs. 50,000!!!
Dar es Salaam: April 9, 2019. Ulikuwa unajiuliza ni wapi na lini unaweza kununua simu mpya, za kisasa na kwa bei nafuu ambayo haukuitegemea?




Katika jitihada za kuhakikisha kuwa inarahisisha upatikanaji na matumizi ya simu za kisasa kwenye maisha ya kila siku ya Watanzania, Jumia imezindua gulio kubwa la mauzo ya simu za mkononi mtandaoni likijulikana kama ‘Mobile Week.’ Hili ni tukio kubwa la mauzo ya bidhaa zinazohusiana na simu ambapo limeanza leo Aprili 8 na kufikia kikomo mnamo Aprili 14. Lengo kuu la kampeni hii ni kuwapatia wateja muda wa kutosha na fursa ya kununua aina tofauti za simu za kisasa wazipendazo kwa bei nafuu, punguzo kubwa la bei, kujipatia vocha za kurahisisha manunuzi pamoja na zawadi kemekem ndani ya kipindi chote cha kampeni.


Akizungumzia sababu zilizopelekea kuwa na kampeni kubwa ya ‘Mobile Week’ kila mwaka, Meneja Masoko wa Jumia Tanzania, Bw. Albany James ameelezea kuwa, “Simu ni miongoni mwa bidhaa ambazo zinanunuliwa zaidi kwenye mtandao wetu wa Jumia. Lakini pia hata kwa takwimu zinazotolewa na Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) zinaonyesha kwamba watumiaji wa simu za mkononi wanaendelea kuongezeka kila mwaka. 
Mwaka 2018 idadi ya watumiaji wa simu walikuwa takribani milioni 43.6 ukilinganisha na milioni 40 mwaka 2017. Hivyo basi sisi kama wadau katika urahisishaji wa mauzo ya bidhaa mbalimbali tumeona ni vema kuwa na kampeni kubwa ya mauzo ya ‘simu pekee’ kila mwaka ambayo itawawezesha Watanzania kufanya manunuzi kwa urahisi na bei nafuu ukilinganisha na sehemu yoyote ile.”


“Mobile Week’ kwetu sisi ni kampeni muhimu zaidi kutokana na manufaa makubwa iliyonayo si tu kwa wateja wetu bali na Watanzania kwa ujumla. Na ndiyo sababu iliyopelekea kila mwaka kujitahidi kuwa wabunifu na kuiboresha kwa kuja na simu za aina tofuati zaidi kutoka kwa washirika wetu, ofa kabambe, punguzo kubwa la bei, vocha za kurahisisha manunuzi pamoja na zawadi kemkem kupitia ‘Treasure Hunt’ siku ya Jumatano ya Aprili 10 kuanzia saa nane mchana. Ambapo simu aina ya Infinix inayouzwa Tshs. 820,000 itauzwa Tshs. 8,000 tu kwa mteja atakayebahatika kuisaka na kuipata kwenye mtandao wetu. Pia kutakuwa na vocha za manunuzi za kila siku ambapo mteja atakuwa anarahisishiwa manunuzi yake pindi atakapozitumia,” aliongezea Bw. James

“Ningependa kutoa wito kwa Watanzania wote kuitumia fursa hii ya ‘Mobile Week’ kununua simu ambazo walikuwa wanatamani kuwa nazo kwani aina ni nyingi na punguzo la bei ni kubwa tofauti na siku za kawaida. Kampeni ya mwaka huu imekuja kitofauti kwasababu kwa manunuzi yoyote ambayo yatazidi Tshs. 50,000 yatakayofanyika kwenye mtandao wa Jumia, mteja atapelekewa bure kabisa bila ya gharama yoyote ya usafirishaji mpaka pale alipo!” Ikipita fursa hii ni mpaka mwakani tena ambapo sidhani kama kuna mtu anaweza kuvumilia kuishi kpindi chote hiko bila ya simu au kuwa tayari kuingia gharama kubwa kufanya manunuzi mara baada ya kampeni hii kupita,” alihitimisha Meneja Masoko wa Jumia Tanzania.


Miongoni mwa sababu zinazopelekea kuendelea kuenea kwa upatikanaji na matumizi ya simu za mkononi na: kuendelea kuongezeka kwa makampuni ya mawasiliano ya simu, kuongezeka kwa makampuni yanayouza simu hivyo kupelekea upatikanaji kuwa rahisi na kwa bei nafuu, pamoja na uwepo wadau wanaorahisisha upatikanaji wa haraka wa bidhaa kama vile Jumia, soko kubwa la uuzaji na manunuzi ya bidhaa mtandaoni.

Tembelea tovuti ya Jumia sasa, https://www.jumia.co.tz/, kujionea bidhaa tofuati zinazopatikana katika kipindi hiki cha kampeni ya ‘Mobile Week’ kabla haijafikia ukomo. Jumia imejizatiti kuhakikisha manunuzi ya uhakika na usalama, urahisi kwa kukutanisha wanunuzi na wauzaji tofauti kutoka sehemu tofauti kwa wakati mmoja, bidhaa ni halisi na za kisasa, bei ni nafuu ukilinganisha na sehemu zingine, na kikubwa zaidi ni kwamba malipo ya bidhaa ni mpaka pale mteja atakapofikiwa na kujiridhisha nazo, na amepewa uwezo wa kuzirudisha na kuomba kubadilishiwa bila ya gharama yoyote ile!


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...