1. Usuli:

Ijumaa ya leo, tarehe 12 April 2019, Taifa letu linatimiza miaka 35 toka kipenzi cha watanzania, marehemu EDWARD MORINGE SOKOINE, afariki kwa ajali ya gari tarehe 12 April 1984 eneo la Dakawa, wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro.

2. Kuzaliwa kwa SOKOINE:

Jumatatu ya tarehe 1 Agosti 1938, katika kitongoji cha Kilasho, kijiji cha Emairete, Monduli Juu, Arusha, huku mvua kubwa ikirindima, alizaliwa mtoto wa kiume aliyekuja kuitwa EDWARD MORINGE SOKOINE. Baba yake aliitwa SOKOINE OLE SEVERE na mama yake aliitwa NAPELEL SINYATI NOOMAYAKI.

3. Elimu:

SOKOINE alisoma Shule ya Msingi Monduli kuanzia mwaka 1949 hadi 1953 na kisha akajiunga na "Monduli Middle School" toka mwaka 1953 hadi 1956. Baada ya hapo alijiunga na Shule ya Sekondari ya Umbwe alikosoma mwaka 1956 hadi 1958.

4. SOKOINE Ajiunga na TANU:

Tarehe 1 Januari 1961,SOKOINE alijiunga na chama cha Tanganyika African National Union (TANU), ikiwa ni miezi michache kabla ya Tanganyika haijapata uhuru.

5. SOKOINE Agombea Ubunge:

Tarehe 25 Octoba 1965, SOKOINE, akiwa kijana mdogo tu wa miaka 27 lakini mwenye akili na ubunifu mkubwa, aligombea na kushinda ubunge jimbo la Monduli.

6. Mh. SOKOINE Aukwaa Uwaziri Mdogo:

Mwaka 1967, Mh.SOKOINE aliteuliwa na Rais NYERERE kuwa Naibu Waziri, Wizara ya Mawasiliano, Usafirishaji na Kazi.

7. Mh. SOKOINE Aukwaa Uwaziri Kamili:

Mwaka 1970, Rais NYERERE, baada ya kuvutiwa na uchapakazi wake, alimteua Mh. SOKOINE kuwa Waziri wa Nchi na mwaka 1972 akamteua kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

8. Mh. SOKOINE Awa Mjumbe wa CC ya CCM:

Baada ya CCM kuzaliwa kutokana na TANU na ASP kuungana tarehe 5 Februari 1977, Mh. SOKOINE akawa mjumbe  wa Kamati Kuu ya CCM.

9. Mh. SOKOINE Ateuliwa kuwa Waziri Mkuu:

Tarehe 13 Februari 1977, kutokana na utendaji kazi wake mujarab, Rais NYERERE alimteua Mh. SOKOINE kuwa Waziri Mkuu.

Hata hivyo, tarehe 7 Novemba 1980, Mh. SOKOINE alijiuzuru na kwenda masomoni Yugoslavia na nafasi yake ikachukuliwa na Mh. CLEOPA DAVID MSUYA.

Baada ya kurejea, Rais NYERERE alimteua tena Mh. SOKOINE kuwa Waziri Mkuu tarehe 24 Februari 1983. Aidha, mwaka huo wa 1983, Mh. SOKOINE alianza kusomea shahada ya "Political Science" Udsm na alikuwa amebakiza sura moja tu umauti ulimpomfika.

10. Mh. SOKOINE "Aliota" kifo chake:

Mh. SOKOINE alihudhuria kikao cha bunge jijini Idodomia mwezi April 1984. Hata hivyo, matendo ya Mh. SOKOINE kabla ya kifo chake yanaashiria huenda alihisi maisha yake duniani yalikuwa yakifikia tamati.

Jumatatu ya tarehe 9 April 1984, Mh. SOKOINE alikwenda kusali kanisa la Mtakatifu PAUL, Idodomia. Usiku wa Jumanne, tarehe 10 April 1984, Mh. SOKIONE aliandaa karamu ya chakula cha jioni kwa Mawaziri na Wakuu wa Mikoa ambapo alionekana kuongea na kila Waziri na kila Mkuu wa Mkoa. Jumatano, tarehe 11 April 1984, aliandaa chakula cha jioni "The Last Supper" kwa Wabunge wote wa mkoani kwake Arusha ambapo aliwasihi wafanye jitihada kuwaondoa wananchi wao kwenye lindi kubwa la ufukara.

11. Mh. SOKOINE Atema Cheche na Kuliaga Bunge:

Mh. SOKOINE, siku ya Jumatano ya tarehe 11 April 1984, akilivunja Bunge, alitiririka:

"Ndugu Spika, ningependa kumalizia kwa kukubaliana na wabunge wote waliosema na ambao hawakusema lakini wana mawazo haya kwamba jambo hili la kutumia fedha bila idhini ya bunge lazima tutafute kila njia ya kulikomesha..... Mungu akipenda tutakutana tena kwenye kikao kijacho cha  bunge. Mimi nasafiri kwa njia ya barabara ili nijionee hali ya mazao ya wakulima...".

12. Mh. SOKOINE Apata Ajali, Afariki:

Mapema Alhamis, tarehe 12 April 1984, Mh.  SOKOINE aliondoka na msafara wake Idodomia akiwa ndani ya Mercedes Benz ambapo msafara huo uliongozwa na gari la polisi. Magari yote yaliyokuwa yakikutana na msafara huo yalikuwa yakipaki pembeni kuupisha.

Baada ya msafara huo kufika eneo la Dakawa, ghafla kilisikika kishindo kikubwa. Gari la Mh. SOKOINE liligongana uso kwa uso na gari aina ya Toyota Landcruiser lililokuwa likiendeshwa na DUMISAN DUBE (23), mpigania uhuru wa chama cha ANC aliyekuwa akiishi Mazimbo, Morogoro. DUBE, licha ya kusimamishwa na polisi, hakusimama kwavile alikuwa kwenye mwendo wa kasi. DUBE, katika Landcruiser hiyo, alikuwa na abiria wawili, Bw. BOYCE MOYE na PERCY GEORGE.

Mh. SOKOINE, ambaye alikuwa amekaa kiti cha nyuma huku hajafunga mkanda, alirushwa na kugonga kioo cha mbele ambapo aliumia sana kifuani na shingoni na kufariki kabla ya kufikishwa hospitali ya serikali mkoani Morogoro ambako madaktari walithibitisha kifo chake.Bw. YUSTO CHUMA, aliyekuwa bodigadi wake aliyekuwa amekaa kiti cha mbele kushoto, aliumizwa vibaya na Bw. ALLY ABDALLAH,ambaye alikuwa ndiye dreva wake, alivunjika mguu.

13. Rais NYERERE Alitangazia Taifa Kifo cha SOKOINE:

Alasiri ya siku hiyo ya alhamis, Radio Tanzania, ikiwa inaendelea na vipindi vyake, ghafla vikasitishwa na wimbo wa Taifa ukapigwa.

Rais NYERERE, baada tu ya wimbo wa Taifa, kwa uchungu mkubwa lakini kwa ujasiri wa hali ya juu, akalitangazia Taifa msiba huo wa kihistoria nchini kama ifuatavyo:

"Ndugu wananchi, leo hii, ndugu yetu, kijana wetu, EDWARD MORINGE SOKOINE, Waziri Mkuu wa Tanzania, alipokuwa akirudi Dar Es Salaam toka Dodoma, gari lake lilipata ajali na amefariki dunia. Ndugu Watanzania, naomba muamini EDWARD amefariki kwa ajali na si kitu kingine".

Mara tu baada ya tangazo hilo, vilio na simanzi vilivyotamalaki nchi nzima "havikuwa vya nchi hii". Aidha, watanzania waliokuwa nje ya nchi nao walibubujikwa na machozi kwa kuondokewa na kipenzi chao. Watanzania kila mahali walikuwa wenye simanzi kubwa. Watu walionekana "dhahir shahir" wamevurugwa!

Kikao cha UWT kilichokuwa kikifanyika Ofisi ya CCM Lumumba kilisambaratika ghafla bila kuahirishwa mara tu Mwenyekiti wake, mama SOPHIA KAWAWA, alipowatangazia wajumbe habari hizo zilizoleta jakamoyo na jitimai kubwa!.

Serikali ikatangaza wiki 2 za maombolezo huku bendera ya Taifa ikipeperushwa nusu mlingoti nchi nzima.

14. Rais NYERERE Aangua Kilio Baada ya Kuuona Mwili wa SOKOINE:

Mwili wa SOKOINE uliwasili Ikulu kutoka Morogoro saa 11 jioni ukiwa umefunikwa bendera ya Taifa. Rais NYERERE, akiongozana na mama MARIA, alijongea kwenye mwili huo na akafunua bendera ya Taifa. Mwalimu akaweka mikono yake miwili kwenye paji la uso wa SOKOINE na yeye na mama MARIA, aliyekuwa na kitambaa cheupe, wakalia kwa uchungu sana hadi kuondolewa na walinzi wao. Kwa wengi, ilikuwa ni mara ya kwanza kumuona Mwalimu akilia hadharani. Kwa hakika, ilikuwa ni siku ya uchungu mkubwa kwa taifa letu kwa jinsi kifo kilivyotokea na hasa kwavile SOKOINE alikuwa akipigiwa chapuo na wengi kuja kuwa Rais wa Tanzania baada ya Mwalimu.

15. JOSEPH NYERERE Azua Kimuhemuhe na Taharuki Ikulu:

JOSEPH NYERERE, mdogo wa Mwalimu, ambaye alijulikana kwa ufyatu wake na kutomun'gunya maneno, ghafla bin vuu, aliingia eneo ulipowekwa mwili huo na kuonekana amefura hasira huku akilia kwa sauti ma kwa uchungu. Ghafla akatamka:
"Mwalimu, huna ulinzi. Waziri Mkuu anakufa barabarani?" . Walinzi wa Ikulu, si tu walimtoa "mkuku" bali pia walihakikisha ameondolewa eneo la Ikulu haraka.!

Mwili wa SOKOINE ukapelekwa hospitali ya Muhimbili kwaajili ya kuhifadhiwa.

16. Jeneza la SOKOINE Latengenezwa Fastafasta Usiku wa Manani:

Shuguli ya kutengeneza jeneza hilo alipewa Bw. GEORGE CHRISTOS (86). Huyu alizaliwa na baba Mgiriki na mama Msukuma aliyeitwa MARIA, aliyekuwa mmoja wa mabinti wa Chifu KIDAHA. Bw. CHRISTOS alikuwa ndiye Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu Tanzania.

Saa 12 jioni siku hiyo, yeye na mkewe, Bi. ELIZABETH WALKER, walitinga Muhimbili ili kuangalia mwili na kuchukua vipimo.

Wakati huo, bohari zote mikoani ilikuwa ni lazma ziwe na majeneza 5 ili ikitokea msiba wa kiongozi kusiwe na tatizo.

SOKOINE alikuwa mtu wa miraba minne "aliyekwenda hewani" hivyo majeneza yote kwenye bohari zote hayakumfaa.

Bw. CHRISTOS, mkewe na Bw. PAUL MKANGA, aliyekuwa Katibu Mkuu Ujenzi, baada ya kupata vipimo, walienda kwenye kiwanda cha HEM SINGH-Chang'ombe ambako walimkuta mwenyewe akiwa katika harakati za kufunga. Kazi ya kulitengeneza jeneza ikaanza mara moja na kumalizika usiku wa manani. Kisha, Bi. WALKER akalipamba jeneza hilo na likapelekwa Muhimbili.

17. SOKOINE Aagwa na Wakazi wa Dsm:

Ijumaa, tarehe 13 April 1984, wakazi wa jiji la Dsm na mikoa ya jirani walifurika kuuaga mwili wa SOKOINE. Kwa hakika, umati huo ulikuwa haujawahi kutokea nchini na rekodi hiyo ilikuja kuvunjwa na msiba wa Baba wa Taifa, Octoba 1999.

18. Daladala Zote Zawapeleka Watu Bure "Airport"

Jumamosi ya tarehe 14 April 1984, mwili wa SOKOINE ulipelekwa "airport" kwaajili ya kusafirishwa kuelekea Arusha. Daladala zote jijini ziliacha "kula vichwa" na badala yake zikawasafirisha wananchi bure kwenda "airport" kama mchango wao kwa kipenzi chao. Ikumbukwe kuwa mwaka 1983, baada ya kuona UDA "inambwelambwela", Mh. SOKOINE ndipo alipoanzisha utaratibu wa "DALADALA", jina lililotokana na neno "Dollar" ambapo "Exchange rate" wakati huo ilikuwa shilingi Tano ambayo ndiyo ilikuwa nauli ya Daladala.

19. SOKOINE Azikwa kwa Heshma Zote:

Kaburi la aina yake la marehemu SOKOINE lilijengwa kwa ustadi mkubwa na Jenerali JOHN BUTLER WARDEN "Black Mamba", Mtanzania Chotara, akisaidiwa na askari wa TPDF.

Kutokana na ubunifu huo wa aina yake, Jenerali WARDEN akapewa heshima ya kujenga kaburi la aliyekuwa Rais wa Msumbiji, SAMORA MOSES MACHEL, ambaye alifariki baada ya ndege yake aina ya Tupulov Tu 134, kuanguka tarehe 19 Octoba 1986.

Mazishi ya SOKOINE yalipewa  heshima zote za kitaifa na yalihudhuriwa na maelfu ya wananchi wakiongozwa na Baba wa Taifa na viongozi toka nje ya nchi.

Miongoni mwa waliohudhuria toka nje ni Mh. OLIVER TAMBO, aliyekuwa Rais wa ANC na Mh. ALFRED NZO aliyekuwa Katibu Mkuu wa ANC ambao walieleza kusikitishwa kwao na ajali hiyo iliyosababishwa na raia mwenzao wa Afrika Kusini.

20. SOKOINE Aacha Wake 2 na  Watoto 11:

SOKOINE alikuwa na wake wawili ambao ni mama NAPONO SOKOINE na mama NAKITETO SOKOINE na watoto 11 wakiwemo Mh. Balozi JOSEPH na Mh. Mbunge NAMELOK.

21. DUMISAN DUBE  Afikishwa kwa Pilato, "Apigwa Mvua 3"

Tarehe 17 Mei 1984, DUMISAN DUBE, aliyesababisha kifo cha SOKOINE, alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Morogoro kwa mara ya kwanza. Kesi hiyo iliahirishwa hadi tarehe 29 Mei 1984.

ANC Tawi la Mazimbo lilimchukua wakili nguli, MOHAMED ISMAIL, kumtetea DUBE. Hata hivyo, ANC HQ Lusaka ilipanga kumtafuta wakili mwingine guru ili kumtetea mpigania uhuru huyo.

Tarehe 12 Juni 1984, upande wa Mashtaka ukiwa "Kamili-Gado" ukiongozwa na  JOHNSON MWANYIKA (SSA) aliyekuwa na mashahidi 21 akiwemo mkulima aliyeshuhudia ajali hiyo,  DUBE aliposomewa tu mashtaka 7 akakiri na Pilato wa wakati huo, Mh. SIMON KAJI (PRM) "akamtwanga mvua 3".

22. SOKOINE Alikuwa Kipenzi Kikubwa cha NYERERE:

Baba wa Taifa alimpenda sana SOKOINE kutokana na uadilifu wake, uchapakazi wake usio wa kawaida, uchamungu wake na ubunifu wake kuntu.

23. Mambo Yaliyofanya SOKOINE Kuwa Kiongozi wa Kipekee na Kupendwa Sana na Watanzania:

23.1 SOKOINE alichukia sana wazembe. "Ole wake Kiongozi mzembe na asiye na nidhamu nitakayemkuta. Viongozi wazembe na wabadhilifu wahesabu siku zao". 26 Machi 1983.

23.2 SOKOINE alitaka wazazi wawajibike kwa watoto  wao- "Vijana wengi leo wana mali kuliko wazee wao waliofanyakazi kwa miaka 40 lakini wazee hao wanataka serikali ndio iwaulize vijana mali wameipata wapi! Hivi kwanini mzazi usimuulize mwanao -"Hii mali umepata wapi"?.

23.3 SOKOINE alihimiza majeshi yawe kwa faida ya wote -  "Katika nchi inayojali haki na usawa, Majeshi hayana budi yawe ni chombo cha kulinda haki na maslahi ya wengi. Kamwe hayaruhusiwi kuwa chombo cha wachache wenye kujali nafsi zao"
1 Februari 1977.

23. 4 SOKOINE alipenda Uzalendo na alikuwa Mzalendo wa kweli kwa nchi yake. "Viongozi wanaoteuliwa lazma wawe Wazalendo. Naskia huko mikoani baadhi ya viongozi wanagombania magari na nyumba. Mambo hayo si muhimu. Viongozi wanatakiwa kugombania juu ya maendeleo ya wanavijiji. Huu ni ugomvi mtakatifu."
11 Desemba 1982.

23.5 SOKOINE alichukia upuuzi. Mwezi Machi 1983, SOKOINE alifanya ziara Singida. Mmoja wa viongozi mkoani humo akamfuata Bw. ACCADOGA CHILEDI aliyekuwa "Press Secretary" wa SOKOINE na kumwambia - "Mzee tumeishamtayarishia Blanketi Chapa ya Binadamu"(akimaanisha Kimada). Bw. CHILEDI akamuuliza Kiongozi huyo- "SOKOINE unamjua au unamsikia? Hilo Blanketi ondoka nalo na toweka hapa haraka, nikimwambia ujue unapoteza kazi yako sasa hivi".

23.6 SOKOINE alikuwa mchapakazi hodari. Daima alifanya kazi hadi usiku na mara nyingine hadi usiku wa manani. Aliwachagua vijana 2 hodari; PHILEMON LUHANJO na MARTENS LUMBANGA waliokuwa chini ya Katibu Mkuu, HORACE KOLIMBA. Hawa watatu walibatizwa jina la "WAFUASI WA SOKOINE" kwani walizunguka nae kote alikoenda na kufuatilia maagizo yote "Bampa tu Bampa".

23. 7 SOKOINE hakupenda utajiri. Maisha yake yalielezewa kwa ufasaha na Mwalimu msibani : "EDWARD hakuwa na mali yoyote ukiachilia mbali ng'ombe wake wa urithi. Alikuwa na suti tatu na viatu pea mbili".

23.8 SOKOINE alikuwa ni mbunifu sana. Alianzisha "PRESIDENTIAL TRUST FUND" Ikulu ambapo alikuwa akiweka sehemu ya mshahara wake ili kuwasaidia akina mama kuweza kukopa!.

23. 9 SOKOINE alikuwa Mchamungu sana. Alikuwa Mkristu mkatoliki na mwanachama wa Utawa wa Tatu wa Mt. Fransisca.

24. NUKUU MUJARAB ZA MH. JPM NA PM KUHUSU SOKOINE:

24.1 "Tarehe 12 April 1984, aliyekuwa Waziri Mkuu, Mh. SOKOINE alipofariki ilikuwa siku ya huzuni kubwa. Mimi nilikuwa JKT Mpwapwa "Operesheni ya Nguvukazi". SOKOINE hatasahaulika Tanzania kwani alipiga vita rushwa, wizi na unyonyaji. Alikuwa Mzakendo wa kweli. Ni wito wangu Watanzania tumuige na tumuishi.."
Mh. JPM, 12 April 2018.

24. 2 "SOKOINE alikuwa Kiongozi bora aliyechukia rushwa na ulanguzi. Hakuwa na ubinafsi, kinyongo wala tamaa ya mali. Namuomba Mungu niwe kama SOKOINE"
Mh. K.MAJALIWA, 12 April 2018.

25. Tafakuri Jadidi:

Je, wewe kama Kiongozi (wa ngazi yoyote ile iwe Kata, darasani au serikalini) unamuenzi na kumuishi marehemu SOKOINE kama alivyotuasa Mh. Rais MAGUFULI?
Jitafakari.

NB: NYIE WOTE MNAOFOWADI ATIKALI ZANGU BAADA YA KUONDOA CHATA LA "ALLEZ LIVERPOOL FC👇 DAWA YENU IPO JIKONI!!.


ALLEZ ALLEZ ALLEZ LIVERPOOL FC!!!🔥🔥🔥KUMBUKIZI YA 35 YA KIFO CHA EDWARD MORINGE SOKOINE


1. Usuli:

Ijumaa ya leo, tarehe 12 April 2019, Taifa letu linatimiza miaka 35 toka kipenzi cha watanzania, marehemu EDWARD MORINGE SOKOINE, afariki kwa ajali ya gari tarehe 12 April 1984 eneo la Dakawa, wilaya ya Mvomero, mkoani Morogoro.

2. Kuzaliwa kwa SOKOINE:

Jumatatu ya tarehe 1 Agosti 1938, katika kitongoji cha Kilasho, kijiji cha Emairete, Monduli Juu, Arusha, huku mvua kubwa ikirindima, alizaliwa mtoto wa kiume aliyekuja kuitwa EDWARD MORINGE SOKOINE. Baba yake aliitwa SOKOINE OLE SEVERE na mama yake aliitwa NAPELEL SINYATI NOOMAYAKI.

3. Elimu:

SOKOINE alisoma Shule ya Msingi Monduli kuanzia mwaka 1949 hadi 1953 na kisha akajiunga na "Monduli Middle School" toka mwaka 1953 hadi 1956. Baada ya hapo alijiunga na Shule ya Sekondari ya Umbwe alikosoma mwaka 1956 hadi 1958.

4. SOKOINE Ajiunga na TANU:

Tarehe 1 Januari 1961,SOKOINE alijiunga na chama cha Tanganyika African National Union (TANU), ikiwa ni miezi michache kabla ya Tanganyika haijapata uhuru.

5. SOKOINE Agombea Ubunge:

Tarehe 25 Octoba 1965, SOKOINE, akiwa kijana mdogo tu wa miaka 27 lakini mwenye akili na ubunifu mkubwa, aligombea na kushinda ubunge jimbo la Monduli.

6. Mh. SOKOINE Aukwaa Uwaziri Mdogo:

Mwaka 1967, Mh.SOKOINE aliteuliwa na Rais NYERERE kuwa Naibu Waziri, Wizara ya Mawasiliano, Usafirishaji na Kazi.

7. Mh. SOKOINE Aukwaa Uwaziri Kamili:

Mwaka 1970, Rais NYERERE, baada ya kuvutiwa na uchapakazi wake, alimteua Mh. SOKOINE kuwa Waziri wa Nchi na mwaka 1972 akamteua kuwa Waziri wa Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa.

8. Mh. SOKOINE Awa Mjumbe wa CC ya CCM:

Baada ya CCM kuzaliwa kutokana na TANU na ASP kuungana tarehe 5 Februari 1977, Mh. SOKOINE akawa mjumbe  wa Kamati Kuu ya CCM.

9. Mh. SOKOINE Ateuliwa kuwa Waziri Mkuu:

Tarehe 13 Februari 1977, kutokana na utendaji kazi wake mujarab, Rais NYERERE alimteua Mh. SOKOINE kuwa Waziri Mkuu.

Hata hivyo, tarehe 7 Novemba 1980, Mh. SOKOINE alijiuzuru na kwenda masomoni Yugoslavia na nafasi yake ikachukuliwa na Mh. CLEOPA DAVID MSUYA.

Baada ya kurejea, Rais NYERERE alimteua tena Mh. SOKOINE kuwa Waziri Mkuu tarehe 24 Februari 1983. Aidha, mwaka huo wa 1983, Mh. SOKOINE alianza kusomea shahada ya "Political Science" Udsm na alikuwa amebakiza sura moja tu umauti ulimpomfika.

10. Mh. SOKOINE "Aliota" kifo chake:

Mh. SOKOINE alihudhuria kikao cha bunge jijini Idodomia mwezi April 1984. Hata hivyo, matendo ya Mh. SOKOINE kabla ya kifo chake yanaashiria huenda alihisi maisha yake duniani yalikuwa yakifikia tamati.

Jumatatu ya tarehe 9 April 1984, Mh. SOKOINE alikwenda kusali kanisa la Mtakatifu PAUL, Idodomia. Usiku wa Jumanne, tarehe 10 April 1984, Mh. SOKIONE aliandaa karamu ya chakula cha jioni kwa Mawaziri na Wakuu wa Mikoa ambapo alionekana kuongea na kila Waziri na kila Mkuu wa Mkoa. Jumatano, tarehe 11 April 1984, aliandaa chakula cha jioni "The Last Supper" kwa Wabunge wote wa mkoani kwake Arusha ambapo aliwasihi wafanye jitihada kuwaondoa wananchi wao kwenye lindi kubwa la ufukara.

11. Mh. SOKOINE Atema Cheche na Kuliaga Bunge:

Mh. SOKOINE, siku ya Jumatano ya tarehe 11 April 1984, akilivunja Bunge, alitiririka:

"Ndugu Spika, ningependa kumalizia kwa kukubaliana na wabunge wote waliosema na ambao hawakusema lakini wana mawazo haya kwamba jambo hili la kutumia fedha bila idhini ya bunge lazima tutafute kila njia ya kulikomesha..... Mungu akipenda tutakutana tena kwenye kikao kijacho cha  bunge. Mimi nasafiri kwa njia ya barabara ili nijionee hali ya mazao ya wakulima...".

12. Mh. SOKOINE Apata Ajali, Afariki:

Mapema Alhamis, tarehe 12 April 1984, Mh.  SOKOINE aliondoka na msafara wake Idodomia akiwa ndani ya Mercedes Benz ambapo msafara huo uliongozwa na gari la polisi. Magari yote yaliyokuwa yakikutana na msafara huo yalikuwa yakipaki pembeni kuupisha.

Baada ya msafara huo kufika eneo la Dakawa, ghafla kilisikika kishindo kikubwa. Gari la Mh. SOKOINE liligongana uso kwa uso na gari aina ya Toyota Landcruiser lililokuwa likiendeshwa na DUMISAN DUBE (23), mpigania uhuru wa chama cha ANC aliyekuwa akiishi Mazimbo, Morogoro. DUBE, licha ya kusimamishwa na polisi, hakusimama kwavile alikuwa kwenye mwendo wa kasi. DUBE, katika Landcruiser hiyo, alikuwa na abiria wawili, Bw. BOYCE MOYE na PERCY GEORGE.

Mh. SOKOINE, ambaye alikuwa amekaa kiti cha nyuma huku hajafunga mkanda, alirushwa na kugonga kioo cha mbele ambapo aliumia sana kifuani na shingoni na kufariki kabla ya kufikishwa hospitali ya serikali mkoani Morogoro ambako madaktari walithibitisha kifo chake.Bw. YUSTO CHUMA, aliyekuwa bodigadi wake aliyekuwa amekaa kiti cha mbele kushoto, aliumizwa vibaya na Bw. ALLY ABDALLAH,ambaye alikuwa ndiye dreva wake, alivunjika mguu.

13. Rais NYERERE Alitangazia Taifa Kifo cha SOKOINE:

Alasiri ya siku hiyo ya alhamis, Radio Tanzania, ikiwa inaendelea na vipindi vyake, ghafla vikasitishwa na wimbo wa Taifa ukapigwa.

Rais NYERERE, baada tu ya wimbo wa Taifa, kwa uchungu mkubwa lakini kwa ujasiri wa hali ya juu, akalitangazia Taifa msiba huo wa kihistoria nchini kama ifuatavyo:

"Ndugu wananchi, leo hii, ndugu yetu, kijana wetu, EDWARD MORINGE SOKOINE, Waziri Mkuu wa Tanzania, alipokuwa akirudi Dar Es Salaam toka Dodoma, gari lake lilipata ajali na amefariki dunia. Ndugu Watanzania, naomba muamini EDWARD amefariki kwa ajali na si kitu kingine".

Mara tu baada ya tangazo hilo, vilio na simanzi vilivyotamalaki nchi nzima "havikuwa vya nchi hii". Aidha, watanzania waliokuwa nje ya nchi nao walibubujikwa na machozi kwa kuondokewa na kipenzi chao. Watanzania kila mahali walikuwa wenye simanzi kubwa. Watu walionekana "dhahir shahir" wamevurugwa!

Kikao cha UWT kilichokuwa kikifanyika Ofisi ya CCM Lumumba kilisambaratika ghafla bila kuahirishwa mara tu Mwenyekiti wake, mama SOPHIA KAWAWA, alipowatangazia wajumbe habari hizo zilizoleta jakamoyo na jitimai kubwa!.

Serikali ikatangaza wiki 2 za maombolezo huku bendera ya Taifa ikipeperushwa nusu mlingoti nchi nzima.

14. Rais NYERERE Aangua Kilio Baada ya Kuuona Mwili wa SOKOINE:

Mwili wa SOKOINE uliwasili Ikulu kutoka Morogoro saa 11 jioni ukiwa umefunikwa bendera ya Taifa. Rais NYERERE, akiongozana na mama MARIA, alijongea kwenye mwili huo na akafunua bendera ya Taifa. Mwalimu akaweka mikono yake miwili kwenye paji la uso wa SOKOINE na yeye na mama MARIA, aliyekuwa na kitambaa cheupe, wakalia kwa uchungu sana hadi kuondolewa na walinzi wao. Kwa wengi, ilikuwa ni mara ya kwanza kumuona Mwalimu akilia hadharani. Kwa hakika, ilikuwa ni siku ya uchungu mkubwa kwa taifa letu kwa jinsi kifo kilivyotokea na hasa kwavile SOKOINE alikuwa akipigiwa chapuo na wengi kuja kuwa Rais wa Tanzania baada ya Mwalimu.

15. JOSEPH NYERERE Azua Kimuhemuhe na Taharuki Ikulu:

JOSEPH NYERERE, mdogo wa Mwalimu, ambaye alijulikana kwa ufyatu wake na kutomun'gunya maneno, ghafla bin vuu, aliingia eneo ulipowekwa mwili huo na kuonekana amefura hasira huku akilia kwa sauti ma kwa uchungu. Ghafla akatamka:
"Mwalimu, huna ulinzi. Waziri Mkuu anakufa barabarani?" . Walinzi wa Ikulu, si tu walimtoa "mkuku" bali pia walihakikisha ameondolewa eneo la Ikulu haraka.!

Mwili wa SOKOINE ukapelekwa hospitali ya Muhimbili kwaajili ya kuhifadhiwa.

16. Jeneza la SOKOINE Latengenezwa Fastafasta Usiku wa Manani:

Shuguli ya kutengeneza jeneza hilo alipewa Bw. GEORGE CHRISTOS (86). Huyu alizaliwa na baba Mgiriki na mama Msukuma aliyeitwa MARIA, aliyekuwa mmoja wa mabinti wa Chifu KIDAHA. Bw. CHRISTOS alikuwa ndiye Mkurugenzi Mkuu wa Bohari Kuu Tanzania.

Saa 12 jioni siku hiyo, yeye na mkewe, Bi. ELIZABETH WALKER, walitinga Muhimbili ili kuangalia mwili na kuchukua vipimo.

Wakati huo, bohari zote mikoani ilikuwa ni lazma ziwe na majeneza 5 ili ikitokea msiba wa kiongozi kusiwe na tatizo.

SOKOINE alikuwa mtu wa miraba minne "aliyekwenda hewani" hivyo majeneza yote kwenye bohari zote hayakumfaa.

Bw. CHRISTOS, mkewe na Bw. PAUL MKANGA, aliyekuwa Katibu Mkuu Ujenzi, baada ya kupata vipimo, walienda kwenye kiwanda cha HEM SINGH-Chang'ombe ambako walimkuta mwenyewe akiwa katika harakati za kufunga. Kazi ya kulitengeneza jeneza ikaanza mara moja na kumalizika usiku wa manani. Kisha, Bi. WALKER akalipamba jeneza hilo na likapelekwa Muhimbili.

17. SOKOINE Aagwa na Wakazi wa Dsm:

Ijumaa, tarehe 13 April 1984, wakazi wa jiji la Dsm na mikoa ya jirani walifurika kuuaga mwili wa SOKOINE. Kwa hakika, umati huo ulikuwa haujawahi kutokea nchini na rekodi hiyo ilikuja kuvunjwa na msiba wa Baba wa Taifa, Octoba 1999.

18. Daladala Zote Zawapeleka Watu Bure "Airport"

Jumamosi ya tarehe 14 April 1984, mwili wa SOKOINE ulipelekwa "airport" kwaajili ya kusafirishwa kuelekea Arusha. Daladala zote jijini ziliacha "kula vichwa" na badala yake zikawasafirisha wananchi bure kwenda "airport" kama mchango wao kwa kipenzi chao. Ikumbukwe kuwa mwaka 1983, baada ya kuona UDA "inambwelambwela", Mh. SOKOINE ndipo alipoanzisha utaratibu wa "DALADALA", jina lililotokana na neno "Dollar" ambapo "Exchange rate" wakati huo ilikuwa shilingi Tano ambayo ndiyo ilikuwa nauli ya Daladala.

19. SOKOINE Azikwa kwa Heshma Zote:

Kaburi la aina yake la marehemu SOKOINE lilijengwa kwa ustadi mkubwa na Jenerali JOHN BUTLER WARDEN "Black Mamba", Mtanzania Chotara, akisaidiwa na askari wa TPDF.

Kutokana na ubunifu huo wa aina yake, Jenerali WARDEN akapewa heshima ya kujenga kaburi la aliyekuwa Rais wa Msumbiji, SAMORA MOSES MACHEL, ambaye alifariki baada ya ndege yake aina ya Tupulov Tu 134, kuanguka tarehe 19 Octoba 1986.

Mazishi ya SOKOINE yalipewa  heshima zote za kitaifa na yalihudhuriwa na maelfu ya wananchi wakiongozwa na Baba wa Taifa na viongozi toka nje ya nchi.

Miongoni mwa waliohudhuria toka nje ni Mh. OLIVER TAMBO, aliyekuwa Rais wa ANC na Mh. ALFRED NZO aliyekuwa Katibu Mkuu wa ANC ambao walieleza kusikitishwa kwao na ajali hiyo iliyosababishwa na raia mwenzao wa Afrika Kusini.

20. SOKOINE Aacha Wake 2 na  Watoto 11:

SOKOINE alikuwa na wake wawili ambao ni mama NAPONO SOKOINE na mama NAKITETO SOKOINE na watoto 11 wakiwemo Mh. Balozi JOSEPH na Mh. Mbunge NAMELOK.

21. DUMISAN DUBE  Afikishwa kwa Pilato, "Apigwa Mvua 3"

Tarehe 17 Mei 1984, DUMISAN DUBE, aliyesababisha kifo cha SOKOINE, alifikishwa Mahakama ya Hakimu Mkazi, Morogoro kwa mara ya kwanza. Kesi hiyo iliahirishwa hadi tarehe 29 Mei 1984.

ANC Tawi la Mazimbo lilimchukua wakili nguli, MOHAMED ISMAIL, kumtetea DUBE. Hata hivyo, ANC HQ Lusaka ilipanga kumtafuta wakili mwingine guru ili kumtetea mpigania uhuru huyo.

Tarehe 12 Juni 1984, upande wa Mashtaka ukiwa "Kamili-Gado" ukiongozwa na  JOHNSON MWANYIKA (SSA) aliyekuwa na mashahidi 21 akiwemo mkulima aliyeshuhudia ajali hiyo,  DUBE aliposomewa tu mashtaka 7 akakiri na Pilato wa wakati huo, Mh. SIMON KAJI (PRM) "akamtwanga mvua 3".

22. SOKOINE Alikuwa Kipenzi Kikubwa cha NYERERE:

Baba wa Taifa alimpenda sana SOKOINE kutokana na uadilifu wake, uchapakazi wake usio wa kawaida, uchamungu wake na ubunifu wake kuntu.

23. Mambo Yaliyofanya SOKOINE Kuwa Kiongozi wa Kipekee na Kupendwa Sana na Watanzania:

23.1 SOKOINE alichukia sana wazembe. "Ole wake Kiongozi mzembe na asiye na nidhamu nitakayemkuta. Viongozi wazembe na wabadhilifu wahesabu siku zao". 26 Machi 1983.

23.2 SOKOINE alitaka wazazi wawajibike kwa watoto  wao- "Vijana wengi leo wana mali kuliko wazee wao waliofanyakazi kwa miaka 40 lakini wazee hao wanataka serikali ndio iwaulize vijana mali wameipata wapi! Hivi kwanini mzazi usimuulize mwanao -"Hii mali umepata wapi"?.

23.3 SOKOINE alihimiza majeshi yawe kwa faida ya wote -  "Katika nchi inayojali haki na usawa, Majeshi hayana budi yawe ni chombo cha kulinda haki na maslahi ya wengi. Kamwe hayaruhusiwi kuwa chombo cha wachache wenye kujali nafsi zao"
1 Februari 1977.

23. 4 SOKOINE alipenda Uzalendo na alikuwa Mzalendo wa kweli kwa nchi yake. "Viongozi wanaoteuliwa lazma wawe Wazalendo. Naskia huko mikoani baadhi ya viongozi wanagombania magari na nyumba. Mambo hayo si muhimu. Viongozi wanatakiwa kugombania juu ya maendeleo ya wanavijiji. Huu ni ugomvi mtakatifu."
11 Desemba 1982.

23.5 SOKOINE alichukia upuuzi. Mwezi Machi 1983, SOKOINE alifanya ziara Singida. Mmoja wa viongozi mkoani humo akamfuata Bw. ACCADOGA CHILEDI aliyekuwa "Press Secretary" wa SOKOINE na kumwambia - "Mzee tumeishamtayarishia Blanketi Chapa ya Binadamu"(akimaanisha Kimada). Bw. CHILEDI akamuuliza Kiongozi huyo- "SOKOINE unamjua au unamsikia? Hilo Blanketi ondoka nalo na toweka hapa haraka, nikimwambia ujue unapoteza kazi yako sasa hivi".

23.6 SOKOINE alikuwa mchapakazi hodari. Daima alifanya kazi hadi usiku na mara nyingine hadi usiku wa manani. Aliwachagua vijana 2 hodari; PHILEMON LUHANJO na MARTENS LUMBANGA waliokuwa chini ya Katibu Mkuu, HORACE KOLIMBA. Hawa watatu walibatizwa jina la "WAFUASI WA SOKOINE" kwani walizunguka nae kote alikoenda na kufuatilia maagizo yote "Bampa tu Bampa".

23. 7 SOKOINE hakupenda utajiri. Maisha yake yalielezewa kwa ufasaha na Mwalimu msibani : "EDWARD hakuwa na mali yoyote ukiachilia mbali ng'ombe wake wa urithi. Alikuwa na suti tatu na viatu pea mbili".

23.8 SOKOINE alikuwa ni mbunifu sana. Alianzisha "PRESIDENTIAL TRUST FUND" Ikulu ambapo alikuwa akiweka sehemu ya mshahara wake ili kuwasaidia akina mama kuweza kukopa!.

23. 9 SOKOINE alikuwa Mchamungu sana. Alikuwa Mkristu mkatoliki na mwanachama wa Utawa wa Tatu wa Mt. Fransisca.

24. NUKUU MUJARAB ZA MH. JPM NA PM KUHUSU SOKOINE:

24.1 "Tarehe 12 April 1984, aliyekuwa Waziri Mkuu, Mh. SOKOINE alipofariki ilikuwa siku ya huzuni kubwa. Mimi nilikuwa JKT Mpwapwa "Operesheni ya Nguvukazi". SOKOINE hatasahaulika Tanzania kwani alipiga vita rushwa, wizi na unyonyaji. Alikuwa Mzakendo wa kweli. Ni wito wangu Watanzania tumuige na tumuishi.."
Mh. JPM, 12 April 2018.

24. 2 "SOKOINE alikuwa Kiongozi bora aliyechukia rushwa na ulanguzi. Hakuwa na ubinafsi, kinyongo wala tamaa ya mali. Namuomba Mungu niwe kama SOKOINE"
Mh. K.MAJALIWA, 12 April 2018.

25. Tafakuri Jadidi:

Je, wewe kama Kiongozi (wa ngazi yoyote ile iwe Kata, darasani au serikalini) unamuenzi na kumuishi marehemu SOKOINE kama alivyotuasa Mh. Rais MAGUFULI?
Jitafakari.





Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...