Na Leandra Gabriel, Blogu ya Jamii
BRIGHT CHABOTA mhitimu wa chuo aliyesomea masuala ya TEHAMA kutoka nchini Afrika Kusini anasakwa na polisi nchini humo kwa tuhuma za kudukua tovuti ya serikali na kujiajiri huku akijilipa mshahara wa donge nono.

Chabota alidukua data za serikali na kujiajiri katika sekta ya afya huku akipokea mshahara bila kufanya kazi kwa miezi 9 kuanzia mwezi Juni mwaka uliopita.

Kijana huyo aligundulika baada ya serikali kukosa rekodi ya malipo kutoka kwake zikiwemo ada ya bima za matibabu hata wazazi wake walipohojiwa walieleza kuwa mtoto wao ameajiriwa na serikali na amekuwa akiwatumia fedha za matumizi. 

Imeelezwa kuwa Chabota alikuwa akijilipa randi 7000 kwa mwezi ambazo ni sawa na shilingi milioni 1.2 kwa mwezi bila kufanya kazi.

Je, udukuzi huu wa Chabota ambaye baba yake ni raia wa Zambia na mama yake akitokea Afrika kusini ni suluhisho kwa vijana waliokosa ajira? nini kifanyike kuhusiana na utaalamu alioufanya kijana huyu?

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...