Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia Prof. Joyce Ndalichako Akizungmza
katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania
na China, iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
Jumatano 24 April 2019.
Balozi wa China Nchini Tanzania Wang Ke, akizungumza katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia Prof. Joyce Ndalichako akisalimiana na
Balozi wa China Nchini Tanzania Wang Ke mara baada ya kumaliza kuhutubia katika
hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na
China, iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano
24 April 2019.
Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia Prof. Joyce Ndalichako, akiteta jambo na
Naibu Waziri wa Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt.Damas
Ndumbaro na Katibu Mkuu CCM, Dkt. Bashiru Ally katika hafla ya Maadhimisho ya
miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika
Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Waziri Mkuu Mstaafu, Mhe. Mizengo Pinda na mkewe Tunu Pinda, wakifuatilia hafla
ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China
iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April
2019.
Katibu Mkuu, Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Faraji
Mnyepe(kushoto), akifuatilia hotuba ya Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia Prof.
Joyce Ndalichako, katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa
kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo
Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Balozi wa China Nchini Tanzania Wang Ke (wa pili kushoto) akifuatilia burudani
katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania
na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
Jumatano 24 April 2019, kushoto kwake ni Waziri wa Elimu Sayansi ya Tekenolojia
Prof. Joyce Ndalichako, Katibu Mkuu CCM, Dkt. Bashiru Ally, Naibu Waziri wa Mambo
ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki, Dkt.Damas Ndumbaro na Waziri wa Katiba
na Sheria, Dkt.Agustine Mahiga.
Wasanii kutoka China wakitoa burudani katika hafla ya Maadhimisho ya miaka
55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba
mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, Jumatano 24 April 2019.
Kikundi cha ngoma za asili kutoka Mwananyamala Jijini Dar es Salaam, kikitoa
Burudani katika hafla ya Maadhimisho ya miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia kati ya
Tanzania na China iliyofanyika katika Maktaba mpya ya Chuo Kikuu cha Dar es Salaam,
Jumatano 24 April 2019.
(Picha na Paschal Dotto-MAELEZO).
Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania na Serikali ya Jamhuri ya Watu wa
China, zimeadhimisha miaka 55 ya uhusiano wa kidiplomasia ulioasisiwa na Hayati
Mwl. Julius Kambarage Nyerere, Rais wa kwanza wa Jamhuri ya Muungano wa
Tanzania na Mao Ze Dong, Rais wa kwanza wa China.
Akiongea katika maadhimisho hayo Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia, Prof. Joyce
Ndalichako, amesema kuwa uhusiano huo umejenga urafiki mkubwa kwa Tanzania na
China katika Nyanja zote za maendeleo.
“Napenda kuanza na Nukuu ya Baba wa Taifa, Mwl. Julius Nyerere ambaye alisema
kuwa “sisi tunataka kuwa rafiki wa kila mtu na hatuwezi kuwa na rafiki ambaye
anatuchagulia adui yetu”, China ilionyesha dhamira ya kuwa rafiki wa Tanzania, rafiki
ambaye tulizuiwa kuwa rafiki yetu kipindi cha ukoloni, maneno haya ya Baba wa Taifa
yalionyesha namna gani alivyokuwa anathamini urafiki wa Tanzania na China, kwa
hiyo China ni rafiki yetu mkubwa”. Amesema Prof. Ndalichako.
Prof. Ndalichako ameeleza kuwa miaka 55 ya uhusiano huo umechochea kuwa na
urafiki mkubwa ambao umeleta faida kwa kila nchi kwa sababu ya kujenga historia
kubwa, kuthaminiana, kuheshimiana, kwa hiyo huo ni urafiki ambao kila mtu
anamuheshimu mwenzie.
Prof.Ndalichako amesema kuwa katika maadhimisho ya miaka 55 kumekuwa na
mafanikio makubwa katika Nyanja ya kiuchumi kwa kuwepo na miradi mbalimbali
inayotokana na uhusiano China na Tanzania, miradi ambayo imetekelezwa ni Reli ya
TAZARA, Kiwanda cha Urafiki, Kiwanda cha UFI, Kiwanda cha dawa keko, Kiwanda cha
sukari Mahonda Zanzibar na Shamba la mpunga Mbarali.
Miradi mingine iliyotekelezwa kwenye urafiki huo ni Uwanja cha mpira wa Taifa,
Uwanja wa mpira Amani Zanzibar, Bwawa la maji Chalinze, Kituo cha Mikutano Julius
Nyerere, Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete, Maktaba ya Chuo Kikuu Dar es Salaam
ambayo ni maktaba kubwa kuliko zote ukanda wa Afrika pamoja na jengo la Wizara ya
Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Afrika Mashariki.
Prof. Ndalichako amesema kuwa China imekuwa ikiifadhili Tanzania nafasi 100 za
wanafunzi kusoma China katika fani mbalimbali zikiwemo za uhandisi na udaktari
“Kila mwaka China imekuwa ikitoa nafasi 100 kwa wanafunzi wetu kusoma nchini
China, lakini pia katika maeneo muhimu kama udaktari kuna nafasi 20 za madaktari
bingwa kwenye fani ya upandikizaji uboho na nafasi 30 kwa madaktari kwenda kusoma
mafunzo mafupi, hakika huu ni urafiki mzuri na umekuwa na mafanikio makubwa”,
amesema Prof.Ndalichako.
Kwa upande wa Miradi ya uwekezaji Prof.Ndalichako amesema kuwa tokea mwaka
1990 hadi Desemba mwaka jana tayari China ina miradi 723 ambayo imefanywa na
wawekezaji kutoka China ambayo imetengeneza ajira 87,126, pia kwenye utalii
Tanzania na China zimekuwa zikishirikiana kwa muda mrefu sasa.
“Tanzania na China zimekuwa na ushirikiano mkubwa pia katika sekta ya utalii na
sekta ya utamaduni, ikiwemo kwa Chuo chetu cha Dar es Salaam na Dodoma kuwa na
taasisi za kufundisha utamaduni wa China, lakini pia tumeanza kufundisha lugha ya
kichina na mpaka sasa shule 15 zinafundisha lugha hiyo, kwenye utalii uzinduzi wa
safari ya ndege yetu ya Dreamliner 787 itaanza safari zake moja kwa moja mpaka
China na kuleta watalii wengi kutoka china kuja kutalii nchini”.
Kwa upande wake Balozi wa China nchini Tanzania, Wang Ke alisema kuwa uhusiano
huo ulioasisiwa na Hayati Mwl. Julius Kambarage Nyerere, Rais wa kwanza wa
Tanzania na Mao Ze Dong Rais wa kwanza wa China, umeleta urafiki mkubwa kwa
watu wa Tanzania na China.
“Hatuna budi kuulinda urafiki huu kwani ni urafiki wa faida, tumekuwa tukishirikiana
katika miradi mbalimabli ikiwemo ujenzi wa reli ya TAZARA na miradi mingine ya
maendeleo ambayo inaleta faida na manufaa kwa watu wetu”, alisema Wang Ke.
Urafiki wa Tanzania na China ulianza mwaka 1964 mara baada ya Tanganyika na
Zanzibar kuungana na kuunda Serikali ya Jamhuri ya Muuungano wa Tanzania.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...