Na, Editha Edward-Tabora 

Watu Watano wa Familia moja katika kijiji cha Isonge Kata ya Sikonge Mkoani Tabora wameuawa na watatu kujeruhiwa baada ya kupigwa na radi iliyoambatana na Mvua na Upepo  mkali 

Tukio hilo lililoibua simazi kubwa limetokea usiku wa saa tano  katika kijiji hicho

Nae kaimu Mathew Sipemba ni kaimu Mganga Mfawidhi Wilaya ya Sikonge amesema alipata taarifa hiyo kutoka polisi juu ya tukio hilo na kukuta watu Watano walikuwa tayari wamepoteza maisha

"Ajali ya radi sio nzuri ni kama moto watu hawa wamejikuta wanavuta hewa ya harufu kali na kuunguza mapafu jambo ambalo limepelekea kupoteza maisha kwa watu hawa"Amesema Sipemba

Kamanda wa polisi mkoa wa Tabora Kamishina msaidizi Emmanuel  Nley amesema Radi hiyo ilisababisha ukuta wa nyumba waliyokuwa wamelala familia hiyo kupasuka na kusababisha vifo hivyo
"Nyumba Ilikuwa imejengwa kwa udongo na makuti na kuezekwa kwa nyasi Mvua iliponyesha  ilisababisha ukuta kupasuka na kupelekea tukio hilo kutokea "Amesema Nley

Kamanda Nley amesema katika tukio hili waliopoteza maisha ni Mhindi Peter, Vailleth Juma, Gress Juma Kulwa Lukanya na Nyanzobe Juma

Peter Nzalalila ni Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge amesema tukio hili lkmeibua simanzi kubwa na amewataka Wananchi wa eneo hilo kuacha kuhusisha tukio hilo na Imani za kishirikina.
Mwenyekiti wa Halmashauri ya Wilaya ya Sikonge Bw. Peter Nzalalila akiongea na Wananchi wa Isongwe

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...