Mkuu wa Kitengo cha
Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari(kulia) akimkabidhi mfano wa hundi ya Sh.
Milioni mbili, Mshindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa
inajulikana kama ‘Cash In Promotion’, Said Khatibu kutoka Zanzibar, jijini Dar
es Salaam jana.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari(kulia)
akimkabidhi mfano wa hundi ya Sh. Milioni mbili, Mshindi wa Promosheni ya
Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’, Mojelwa
Mlinga kutoka Dar es Salaam kwenye hafla iliyofanyika makao makuu ya Tigo,
jijini Dar es Salaam jana
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James
Sumari(katikati) akiwapongeza kwa kuwanyanua mikono juu washindi wa Promosheni
ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’. Kulia
ni Mojelwa Mlinga kutoka Dar es Salaam na kushoto Said Khatibu kutoka Zanzibar
Washindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa
ikijulikana kama ‘Cash In Promotion’.Said Khatibu (kushoto) kutoka Zanzibar na
Mojelwa Mlinga kutoka Dar es Salaam na (kulia) wakifurahia mfano wa hundi
walizabidhiwa baada ya kuibuka washindi katika promosheni hiyo.
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James
Sumari(katikati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) muda mfupi
kabla ya kukabiudhi zawadi kwa washindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa
iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’,Kulia ni Mojelwa Mlinga, mshindi
kutoka Dar es Salaam na kushoto Said Khatibu kutoka Zanzibar.
Kampuni
ya Tigo Tanzania, leo imetoa zawadi za mamilioni ya shilingi kwa
mawakala wake wa huduma ya Tigo Pesa kupitia promosheni iliyomalizika
hivi karibuni ya ‘Wakala Cash In Promotion’.
Promosheni hiyo ya
nchi nzima ilianza Machi 1 na kumalizika Machi 31 ikilenga kuwahamasisha
mawakala wa Tigo Pesa kufanya miamala zaidi na wateja ili kujishindia
zawadi za fedha taslimu.
Akizungumza wakati wa kutoa zawadi kwa
baadhi ya washindi jijijni Dar es Salaam jana,mkuu wa kitengo cha bidhaa
wa Tigo Pesa James Sumari alisema jumla ya Mawakala 97,000 walishiriki
katika promosheni hiyo ya mwezi mmoja.
“Promosheni hii ya aina
yake, ni ya saba kwa Mawakala wetu. Tangu tulipoanza hadi kufikia hivi
sasa, tumewazawadia mawakala 12,000 zaidi ya fedha taslimu shilingi
bilioni 1. Washindi hawa wametoka kila kanda hapa nchini na tumeendelea
kuona mwitikio mkubwa wa Mawakala kupitia promosheni hii na ni mpango
wetu kuendelea kuwarushia tunachokipata kupitia wao wakati tukiendela na
safari ya kufikisha huduma jumuifu za kifedha nchi nzima,” alisema
Sumari
Kwa mujibu wa Sumari, Promosheni ya mwaka huu,
ilishuhudia washindi wakubwa 8 kutoka sehemu mbali mbali za nchi ambao
waliweza kujishindia fedha zaidi kutokana kuwa washindi wa jumla kwenye
promosheni.
“Tumechagua Mawakala wawili waliofanya vizuri
kuliko wengine katika kanda zote nne na kuwazawadia kutokana na jitihada
zao za kufanya miamala mingi zaidi na wateja. Leo pia tunawashindi
ambao watapata zawadi zaidi za fedha taslimu.
Washindi wakubwa
ambao leo wanakabidhiwa zawadi zao wanatokea kanda ya Pwani ambao ni
pamoja na Said Khatib kutoka Zanzibar ambaye atakabidhiwa shilingi
milioni 2 na Mojelwa Mlinga Mojelwa kutoka Dar es Salaam ambaye
amejinyakulia Shilingi milioni 1.
Tunayo furaha kuhitimisha
promosheni yetu kwa kishindo.Tunaamini fedha tulizowazawadia Mawakala
wetu zitawasaidia kukuza biashara zao pamoja na kukidhi mahitaji yao
mengine. Napenda kumalizia kwa kumpongeza bwana Khatib na Mojewa pamoja
na maelfu ya washindi wengine. Mchango wao unatusaidia kuweza kufikisha
huduma jumuifu za kifedha hapa Tanzania kupitia Tigo Pesa,” alifafanua
Sumari.
Sumari aliongeza kuwa, makabidhiano ya zawadi kwa
washindi wa jumla katika kanda za Kaskazini, Kusini na Kanda ya Ziwa
yatafanyika baadaye mwezi huu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...