Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari(kulia) akimkabidhi mfano wa hundi ya Sh. Milioni mbili, Mshindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’, Said Khatibu kutoka Zanzibar, jijini Dar es Salaam jana.

Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari(kulia) akimkabidhi mfano wa hundi ya Sh. Milioni mbili, Mshindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’, Mojelwa Mlinga kutoka Dar es Salaam kwenye hafla iliyofanyika makao makuu ya Tigo, jijini Dar es Salaam jana
Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari(katikati) akiwapongeza kwa kuwanyanua mikono juu washindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’. Kulia ni Mojelwa Mlinga kutoka Dar es Salaam na kushoto Said Khatibu kutoka Zanzibar

Washindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa ikijulikana kama ‘Cash In Promotion’.Said Khatibu (kushoto) kutoka Zanzibar na Mojelwa Mlinga kutoka Dar es Salaam na (kulia) wakifurahia mfano wa hundi walizabidhiwa baada ya kuibuka washindi katika promosheni hiyo. 

Mkuu wa Kitengo cha Bidhaa wa Tigo Pesa, James Sumari(katikati) akiongea na waandishi wa habari (hawapo pichani) muda mfupi kabla ya kukabiudhi zawadi kwa washindi wa Promosheni ya Mawakala wa Tigo Pesa iliyokuwa inajulikana kama ‘Cash In Promotion’,Kulia ni Mojelwa Mlinga, mshindi kutoka Dar es Salaam na kushoto Said Khatibu kutoka Zanzibar.






Kampuni ya Tigo Tanzania, leo imetoa zawadi za mamilioni ya shilingi kwa mawakala wake wa huduma ya Tigo Pesa kupitia promosheni iliyomalizika hivi karibuni ya ‘Wakala Cash In Promotion’. 

Promosheni hiyo ya nchi nzima ilianza Machi 1 na kumalizika Machi 31 ikilenga kuwahamasisha mawakala wa Tigo Pesa kufanya miamala zaidi na wateja ili kujishindia zawadi za fedha taslimu. 

Akizungumza wakati wa kutoa zawadi kwa baadhi ya washindi jijijni Dar es Salaam jana,mkuu wa kitengo cha bidhaa wa Tigo Pesa James Sumari alisema jumla ya Mawakala 97,000 walishiriki katika promosheni hiyo ya mwezi mmoja. 

“Promosheni hii ya aina yake, ni ya saba kwa Mawakala wetu. Tangu tulipoanza hadi kufikia hivi sasa, tumewazawadia mawakala 12,000 zaidi ya fedha taslimu shilingi bilioni 1. Washindi hawa wametoka kila kanda hapa nchini na tumeendelea kuona mwitikio mkubwa wa Mawakala kupitia promosheni hii na ni mpango wetu kuendelea kuwarushia tunachokipata kupitia wao wakati tukiendela na safari ya kufikisha huduma jumuifu za kifedha nchi nzima,” alisema Sumari 

Kwa mujibu wa Sumari, Promosheni ya mwaka huu, ilishuhudia washindi wakubwa 8 kutoka sehemu mbali mbali za nchi ambao waliweza kujishindia fedha zaidi kutokana kuwa washindi wa jumla kwenye promosheni. 

“Tumechagua Mawakala wawili waliofanya vizuri kuliko wengine katika kanda zote nne na kuwazawadia kutokana na jitihada zao za kufanya miamala mingi zaidi na wateja. Leo pia tunawashindi ambao watapata zawadi zaidi za fedha taslimu. 

Washindi wakubwa ambao leo wanakabidhiwa zawadi zao wanatokea kanda ya Pwani ambao ni pamoja na Said Khatib kutoka Zanzibar ambaye atakabidhiwa shilingi milioni 2 na Mojelwa Mlinga Mojelwa kutoka Dar es Salaam ambaye amejinyakulia Shilingi milioni 1. 

Tunayo furaha kuhitimisha promosheni yetu kwa kishindo.Tunaamini fedha tulizowazawadia Mawakala wetu zitawasaidia kukuza biashara zao pamoja na kukidhi mahitaji yao mengine. Napenda kumalizia kwa kumpongeza bwana Khatib na Mojewa pamoja na maelfu ya washindi wengine. Mchango wao unatusaidia kuweza kufikisha huduma jumuifu za kifedha hapa Tanzania kupitia Tigo Pesa,” alifafanua Sumari. 

Sumari aliongeza kuwa, makabidhiano ya zawadi kwa washindi wa jumla katika kanda za Kaskazini, Kusini na Kanda ya Ziwa yatafanyika baadaye mwezi huu. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...