Katika jitihada za kutafutia Watanzania nafasi za masomo nje ya nchi, Ubalozi wa Tanzania nchini Malaysia umefanikiwa kupata ufadhili (scholarships) kwa wanafunzi 160 katika fani mbalimbali. 



Kwa mujibu wa Balozi wa Tanzania nchini Malaysia, Dkt Ramadhani Dau, Ufadhili huo ambao umetolewa na Chuo Kikuu cha UNISEL (University of Selangor) kilichopo Kuala Lumpur una thamani ya USD 1,851,860 sawa na shs 4,287,084,410 za Tanzania.

Dkt. Dau amesema ufadhili huo wa masomo utahusu fani zifuatazo:

1. Bachelor of Civil Engineering 

2. Bachelor of Electrical Engineering 

3. Bachelor of Mechanical Engineering 

4. Bachelor of Occupational Health and Safety 

5. Bachelor of Medical Laboratory 

6. Bachelor of Industrial Biotechnology 

7. Bachelor of Computer Science 

8. Bachelor of Information Technology 

Chuo Kikuu cha Selangor ni miongoni mwa vyuo vya Serikali ambacho kilianzishwa mwaka 1999 na kina program za masomo zaidi ya 90 kwenye ngazi mbalimbali kuanzia stashahada hadi shahada ya uzamivu (PhD).  Kwa sasa UNISEL ina wanafunzi
13,500 

 Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Ramadhani Dau akipokea barua rasmi ya ufadhili huo wa masomo kutoka kwa Profesa Dkt. Mohammad Ridhwan Othman wa 
Chuo Kikuu cha UNISEL University of Selangor jijini Kuala Lumpur leo
Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Ramadhani Dau akipokea barua rasmi ya ufadhili huo wa masomo kutoka kwa Profesa Dkt. Mohammad Ridhwan Othman wa 
Chuo Kikuu cha UNISEL University of Selangor jijini Kuala Lumpur leo
 Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Ramadhani Dau akiwa katika picha ya pamoja baada ya kukabidhiwa barua rasmi ya ufadhili huo wa masomo kutoka kwa Profesa Dkt. Mohammad Ridhwan Othman wa Chuo Kikuu cha UNISEL University of Selangor jijini Kuala Lumpur leo
 Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Ramadhani Dau akitembezwa kwenye maeneo mbalimbali ya chuo baada ya kukabidhiwa barua rasmi ya ufadhili huo wa masomo kutoka kwa Profesa Dkt. Mohammad Ridhwan Othman wa Chuo Kikuu cha UNISEL University of Selangor jijini Kuala Lumpur leo
Balozi wa Tanzania nchini Malaysia Dkt. Ramadhani Dau akitembezwa kwenye maeneo mbalimbali ya chuo baada ya kukabidhiwa barua rasmi ya ufadhili huo wa masomo kutoka kwa Profesa Dkt. Mohammad Ridhwan Othman wa Chuo Kikuu cha UNISEL University of Selangor jijini Kuala Lumpur leo


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...