Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba akiongea na wawakilishi kutoka taasisi mbalimbali ambao kwa pamoja wanaunda kikosi kazi cha kusimamia utekelezaji wa katazo la mifuko ya plastiki hapa nchini. Wajumbe hao ni kutoka Baraza la Taifa la Hifadhi na Usimamizi wa Mazingira (NEMC), Mamlaka ya Mapato Tanzania, Idara ya Uhamiaji, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, Shirika la Viwango Tanzania, Mamlaka ya Chakula na Dawa, Jeshi la Polisi, Ofisi ya Mkemia Mkuu wa Serikali na Ofisi ya Rais Tawala za Mikoa na Serikali za Mitaa. Kikao hicho kimefanyika hii leo katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango – Dodoma.
Sehemu ya wajumbe wanaounda kikosi kazi cha kusimamia utekelezaji wa katazo la mifuko ya plastiki hapa nchini wakimsikiliza Waziri wa Nchi Ofisi ya Makamu wa Rais Muungano na Mazingira Mhe. January Makamba (Hayupo pichani) wakati wa kikao kazi kilichofanyika hii leo katika Ukumbi wa Chuo cha Mipango.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...