Mabaki ya mwili wa aliyekuwa kiongozi wa waasi wa Angola, Jonas Savimbi, yatazikwa tena kwenye mji wake wa Lopitanga mwezi ujao.

Taarifa iliyotolewa jana (Mei 20) na Waziri wa Nchi hiyo Pedro Sebastiao ilieleza kuwa mazishi hayo yangelifanyika baada ya vipimo vya vinasaba kuthibitisha kuwa mabaki hayo ni ya Savimbi.

Savimbi, ambaye alipigana dhidi ya serikali ya Kisoshalisti ya Angola katika vita vya wenyewe kwa wenyewe vya miaka 27, aliuawa Februari 22 mwaka  2002 katika mapambano dhidi ya vikosi vya MPLA.

Kifo chake kilifungua njia ya kufikiwa makubaliano ya amani ambayo yalimaliza moja kati ya mizozo ya muda mrefu kabisa Barani Afrika, ambao ulizuka baada ya Angola kupata uhuru wake kutoka Ureno mwaka 1975.

Savimbi alizikwa siku moja baada ya kuuawa katika Jimbo la Mashariki la Moxico.Vipimo vya vinasaba vilivyofanyika katika Maabara za Afrika Kusini, Argentina, Ureno na Angola vilithibitisha kuwa mabaki hayo ni ya mwili wa Savimbi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...