Waziri wa Nishati Medard Kalemani akionyesha moja ya Mita ambazo zinaweza kutumika kwa mwananchi wa kawaida katika matumizi ya nyumbani ikiwemo kutumika kwenye taa,jiko,friji na matumizi mwengine ambayo alikwenda nazo za bure 
Waziri wa Nishati Medard Kalemani akiwa amezungukwa na wananchi wa Digodigo kama inavyoonekana kwenye picha ,pembeni yake anaonekana Naibu waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia Willium Tate Olenasha ambae pia ni Mbunge wa Ngorongoro.
Waziri wa Nishati Medard Kalemani akionyesha moja ya Mita ambazo zinaweza kutumika kwa mwananchi wa kawaida katika matumizi ya nyumbani ikiwemo kutumika kwenye taa,jiko,friji na matumizi mengine hapa akimkabidhi mwananchi mita hiyo bure.
Waziri wa Nishati akitolea ufafanuzi jambo kwa wananchi wa Dogodigo.
Naibu Waziri wa Elimu Sayansi na Teknolojia William Tate Olebasha akisalimia na wananchi wa Digodigo kama inavyoonekana pichani. 
Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalimani akisalimiana na wananchi wa Digodigo wilayani Ngorongoro ambapo alikwenda huko kwaajili ya uzinduzi wa awamu ya tatu ya umeme wa Rea umefanyika Kimkoa katika Mkoa wa Arusha. 
Mkuu wa mkoa wa Arusha Mrisho Gambo akizungumza na wananchi wa Digodigo wilayani Ngorongoro ambapo umeme wa Rea awamu ya tatu umezinduliwa Kimkoa na Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani.
Meneja wa Tanesco Mkoa wa Arusha Injinia Herini Mhina 
Mhandisi wa Miradi ya REA Nchini John Kitonga
Kutoka kulia ni Meneja wa Tanesco Mkoa wa Arusha Herini Mhina akifiatiwa na Meneja wa Tanesco wilaya ya Ngorongoro Domonic Shahid walipokuwa wakitambulishwa kwa wananchi katika Kata ya Dogodigo ,kijiji cha digodigo wilaya ya Ngorongoro. 
Kutoka kulia ni Meneja wa Tanesco Mkoa wa Arusha Herini Mhina akifiatiwa na Meneja wa Tanesco wilaya ya Ngorongoro Domonic Shahid,Msimamizi wa Rea Tanesco Gesto Jindwa, walipokuwa wakitambulishwa kwa wananchi katika Kata ya Dogodigo ,kijiji cha digodigo wilaya ya Ngorongoro
Kutoka kulia ni Meneja wa Tanesco Mkoa wa Arusha Herini Mhina akifiatiwa na Meneja wa Tanesco wilaya ya Ngorongoro Domonic Shahid,Msimamizi wa Rea Tanesco Gesto Jindwa, Wengine ni wakandarasi Wakandarasi wa kampuni ya Nipo Group wanaotekelea mradi huo walipokuwa wakitambulishwa kwa wananchi katika Kata ya Dogodigo ,kijiji cha digodigo wilaya ya Ngorongoro
Waziri wa Nishati Medard Kalemani akiwahutubia wananchi wa Kata ya Digodigo wilaya ya Monduli mkoa wa Arusha alipokwenda kuwasha umeme awamu ya tatu wa Rea ambapo uzinduzi huo umefanyika kimkoa.
Wanafunzi wa Shule ya Sekondari Digodigo wakimpokea Waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani alipotembelea Shuleni hapo.
Waziri wa Nishati Dkt Mesard Kalemani akizungumza na wanagunzi wa Shule ya Sekondari Digodigo ambapo amewataka kusoma kwa bidii muda na wasichezee Elimu kwani muda wa mapenzi kwao bado sana.Habari/ Picha na Vero Ignatus -Michuzi TV.



Na.Vero Ignatus,Ngorongoro.

Ni zaidi ya kilometa 400 kutoka Arusha Mjini hadi kufikia kata ya Digodigo iliyopo wilaya ya ngorongoro ambayo umezinduliwa umeme wa awamu ya Tatu REA Kimkoa na kuwashwa katika maeneo mbalimbali wilayani humo.

Akizindua Mradi huo waziri wa Nishati Dkt.Medard Kalemani amesema serikali imetoa zaidi ya Sh.bilioni 40 kwa ajili ya umeme, hivyo vema kila mwananchi ahakikishe anawasha nyumbani kwake umeme kabla ya kulazimishwa,kwani umeme huo umepelekwa kupitia Wakala wa umeme vijijini REA.

"Serikali imetumia fedha nyingi hizi sasa sio mchezo watu tuache kuunganisha umeme katika nyumba zenu msisubiri tuwalazimishe,"alisema tutatumia zaidi ya Sh.bilioni 20 katika miradi hiyo ya umeme.Dkt.Kalemani ametoa agizo kwa wakandarasi wa kampuni ya Nipo Group kuongeza kasi katika utendaji wasibweteke kwani mradi huko awali ulisuasua hivyo ifikapo 30 ndiyo mwisho wa kazi zao maeneo hayo.Amewaagiza kuhakikisha vijiji vyote na vitongoji vinapata umeme,amesema kisirukwe kijiji hata kimoja bila kupata umeme na utekelezaji ufanyike chini ya uangalizi wa mwenyekiti wa kijiji husika na kitongoji. 

Dkt.Kalemani amemtaka Meneja wa mkoa wa Tanesco Mhandisi Herini Mhina kuhakikisha anatatua malalamiko ya kukatika kwa umeme katika Jiji la Arusha mara kwa mara na kuhakikisha kila wilaya umeme unafika nyumba hadi nyumba.Pia aliagiza Wakandarasi hao kuajiri vibarua wasiopungua 60 ili kazi niende kwa haraka na wakati huo watasaidia Serikali kuboresha maisha ya wananchi.

"Serikali imewalipa na nyie waajiri watu wa maeneo haya na muwalipe ili kuboresha maisha yao,"alisema.Kuhusu nguzo kutoza wananchi gharama alipiga marufuku kwa kampuni hiyo na Mameneja wa Tanesco kusimamia hilo.Mrisho Gambo ni Mkuu wa mkoa wa Arusha amesema kuwa tangia kupata uhuru wilaya ya ngorongoro haijawahi kuwa na hospitali ya wilaya ila sasa inajengwa ambapo mil.400 zimetengwa kwaajili hiyo,barabara kiwango cha lami kwa sasa imeanzwa kutengenezwa km 50 ikiwa itekelezaji wa majukumu ya serikali ya awamu ya tano.

Gambo amewataka wananchi waweze kutandaza nyaya kwenye nyumba zao ili wapate huduma ya umeme kwa bei nafuu ya elfu 27 kwani wakichelewa watakuja kufungiwa kwa bei kubwa zaidi.

Naye Naibu Waziri wa Elimu,Sayansi na Teknolojia Willium Ole Nasha ameishukuru Serikali kupeleka umeme Ngorongoro na kuzindua rasmikwani katika kipindi cha Serikali ya sasa imejitahidi kupeleka maendeleo mengi katika Wilaya hiyo ambayo hawajawahi kutekelezwa tangu Uhuru kupatikana.

Amesema katika hali ya kawaida Ngorongoro hawakuwahi kufikiria kama watapata umeme.hivyo yeye kama mbunge wao anewataka wananchi hao kujitahidi kutumia umeme huo kujiletea maendeleo.Kwa upande wake Ambilikile Mwasapila (Babu wa Kikombe) alishukuru Serikali kumwashia umeme nyumbani kwake."Lakini hii ishara ya kutimia kwa ndoto zake anayoonyeshwa na Mungu kila mara kuwa Tanzania ni kioo cha Afrika sasa hizi ndizo ishara zimeanza kuonekana,"alisema.

Mbali na kuwasha umeme nyumbani kwa Babu wa kikombe,pia aliwasha Kituo cha Afya Digodigo,Shule ya Msingi Bisikene iliyopo Kata ya Digodigo na Ofisi ya Afisa Tarafa Digodigo

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...