Mkuu wa mauzo wa kanda ya Dar na Pwani wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc, George Lugata (aliyelala chini) na Msimamizi wa mifumo ya kompyuta Emmanuel Lenduyayi (aliyesimama) akitoa mfano wa namna ya kumhudumia mtu aliyeanguka ghafla katika semina ya mafunzo ya huduma ya kwanza, yaliyofanyika makao makuu ya kampuni jijini Dar es Salaam karibuni jijini Dar es Salaam. Kampuni ya Vodacom hutoa mafunzo mbalimbali ya uokoaji kwa wafanyakazi wake na wafanyakazi wa majumbani kwao ili kuwawezesha kukabiliana na ajali mbalimbali ikiwa ni jitihada za kampuni hiyo kuhakikisha usalama wa wafanyakazi wake. Aliyesimama kulia ni mwalimu wa mafunzo hayo Bw Adam kutoka kampuni ya Knight Support Company.

Mfanyakazi wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc Neema Mgombelo, akionyesha mfano wa jinsi ya kumtambua mgonjwa aliezimia katika semina ya mafunzo ya huduma ya kwanza, iliyofanyika makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam hivi karibuni. Kampuni ya Vodacom hutoa mafunzo mbalimbali ya uokoaji kwa wafanyakazi wake na wafanyakazi wa majumbani kwao ili kuwawezesha kukabiliana na ajali mbalimbali ikiwa ni jitihada za kampuni hiyo kuhakikisha usalama wa wafanyakazi wake. Kushoto ni Mwalimu wa mafunzo hayo Bw Adam kutoka kampuni ya Knight Support Company.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...