Mkuu
wa mauzo wa kanda ya Dar na Pwani wa kampuni ya Vodacom Tanzania
Plc, George Lugata (aliyelala chini) na Msimamizi wa mifumo ya kompyuta
Emmanuel Lenduyayi (aliyesimama) akitoa mfano wa namna ya kumhudumia mtu
aliyeanguka ghafla katika semina ya mafunzo ya huduma ya kwanza,
yaliyofanyika makao makuu ya kampuni jijini Dar es Salaam karibuni
jijini Dar es Salaam. Kampuni ya Vodacom hutoa mafunzo mbalimbali ya
uokoaji kwa wafanyakazi wake na wafanyakazi wa majumbani kwao ili
kuwawezesha kukabiliana na ajali mbalimbali ikiwa ni jitihada za kampuni
hiyo kuhakikisha usalama wa wafanyakazi wake. Aliyesimama kulia ni
mwalimu wa mafunzo hayo Bw Adam kutoka kampuni ya Knight Support
Company.
Mfanyakazi
wa kampuni ya Vodacom Tanzania Plc Neema Mgombelo, akionyesha mfano wa
jinsi ya kumtambua mgonjwa aliezimia katika semina ya mafunzo ya huduma
ya kwanza, iliyofanyika makao makuu ya kampuni hiyo jijini Dar es Salaam
hivi karibuni. Kampuni ya Vodacom hutoa mafunzo mbalimbali ya uokoaji
kwa wafanyakazi wake na wafanyakazi wa majumbani kwao ili kuwawezesha
kukabiliana na ajali mbalimbali ikiwa ni jitihada za kampuni hiyo
kuhakikisha usalama wa wafanyakazi wake. Kushoto ni Mwalimu wa mafunzo
hayo Bw Adam kutoka kampuni ya Knight Support Company.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...