Na Seif Mangwangi, Arusha
KIWANDA cha A to Z cha jijini hapa kimeingia mkataba wa bilioni 3.5 wa kuzalisha dawa aina ya AFLASAFE ya kutibia mazao yanayosababisha sumukuvu inayopatikana kwenye mahindi na karanga na ambayo imekuwa ikisababisha maradhi ya saratani ya ini.
Mbali ya saratani ya ini, Sumukuvu (AFLATOX), inaelezwa kusababisha kudumaa kwa watoto ambao wamekuwa wakinywa uji unaotumia unga unaotengenezwa kwa zao la mahindi pamoja na karanga kwaajili ya lishe
Mtendaji Mkuu wa A to Z, Kalpesh Shah na Kaimu Mkurugenzi wa taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo (IITA) yenye makao yake makuu nchini Nigeria, Dkt Kenton Dashell walisema dawa hiyo itakuwa ni suluhu ya maradhi ya saratani kwa kuwa yamekuwa yakisababisha vifo vingi kwa wananchi wa Afrika.
DKT Dashell alisema kila mwaka maelfu ya waafrika wamekuwa wakipoteza maisha kwa maradhi yanayosababishwa na sumukuvu na kupoteza nguvu kazi ya mataifa mengi ya Afrika, hivyo kuzalishwa kwa dawa hiyo kutapunguza vifo na kukuza uchumi wa Afrika.
“ Kati ya kampuni nyingi zilizotenda kuomba mradi wa kuzalisha dawa hii, ni A to Z pekee ndio iliyoonekana kuwa na sifa na uwezo wa kuizalisha, kwa hiyo nipende tu kuwapongeza  sana kwa kushinda tendaII H,”alisema.
Kwa upande wake Mtendaji Mkuu wa A to Z, Kalpesh Shah alisema kampuni yake itatumia Bilioni 3.5 katika mradi huo na kwamba dawa  hiyo itakayokuwa ikijulikana kama Aflasafe TZ01, itaanza kutumika nchini Novemba mwaka huu baada ya uzalishaji kuanza rasmi.
Alisema kwa miaka mingi A to Z imekuwa ikifanya utafiti wa kugundua dawa ya kutibu Sumukuvu kupitia taasisi yake ya utafiti ya ATRC, kwa kuwa sumu hiyo imekuwa ikiwasababishia wakulima hasara kubwa pamoja na kupoteza soko la mazao yao nje ya nchi, hivyo kugunduliwa kwa dawa hiyo na wao kupata fursa ya kuizalisha ni jitihada za muda mrefu za kuokoa vifo na kukuza uchumi wa Tanzania na Afrika.

  Mtendaji Mkuu wa A TO Z Kalpesh Shah akitambulisha dawa aina ya Aflasafe ambayo itatumika kunyunyiziwa kwenye mahindi na karanga kwaajili ya kuua sumukuvu ambayo imekuwa ikisababisha maradhi ya saratani ya ini.
Kaimu Mkurugenzi wa taasisi ya kimataifa ya utafiti wa mazao ya kilimo (IITA), Dkt Kenton Dashell pamoja na Mtendaji Mkuu wa ATOZ Kalpesh Shah wakibadilishana nyaraka za makubaliano ya kuanza uzalishaji wa sawa aina ya Aflasafe kwaajili ya kuua sumukuvu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...