Imeelezwa kuwa Upungufu wa
wataalamu wa kutosha wa kutoa huduma za dawa ya usingizi na ganzi umekuwa
ukisababisha changamoto kwa wagonjwa kukosa huduma stahiki.
Hayo yamesemwa na Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa
Muhimbili, Prof Laurence Museru wakati wa Mkutano uliowakuwanisha wataalamu wa
kutoa huduma za dawa ya usingizi na ganzi wa ndani na nje ya nchi.
Prof. Museru amesema kuwa wataalam wa kutoa dawa hizo kwa Tanzania
wapo 40 ambapo mpaka kufikia mwishoni mwa mwaka huu watafika 50.
“Hapo awali nchini kulikuwa na wataalam 10 na baadae wakaongezeka
na kufikia 40 ila huitaji tunaitaji kufikia wataalam 200”. Amesema museru.
Ameongeza kuwa serikali imekuwa ikiongeza juhudi kwa kuwasomesha
wauguzi ili kuzidi kuboresha huduma hiyo.
Pia amesema kumekua na ongezeko la ajali hivyo kupitia wataalam
waliopo na watakao ongezeka watasaidia kuhuisha majeruhi mahututi na wanopoteza
fahamu.Naye Rais wa chama cha watoa huduma wa dawa za usingizi na ganzi
SATA, Dk. Mpoki Ulisubisya amesema lengo la mkutano huo ni kuweza kuweza
kuboresha huduma na kuona ni namna gani tunaweza kutoa elimu ili kuongeza
wataalam.
“Tutakuwa tukiweka ushawishi kwa vijana kuweza kusomea ili kuongeza
idadi yetu y’all madaktari kwani kwa nchi nzima atufiki 50 ivyo tunataka tuwe
wengi”. Amesema Dkt. Mpoki.Pia Dk. Mpoki aliongeza kuwa nia yao kila hospitali ya rufaa na
mkoa kuwa na angalau daktari bingwa mmoja.
Balozi Dkt Ulisubisya Mpoki akifungua Mkutano wa wataalamu wa kutoa huduma za dawa ya usingizi na ganzi iliyofanyikakwenye hoteli ya Peacock jijini Dar es salaam.
Mkurugenzi Mtendaji wa Hospitali ya Taifa Muhimbili, Prof Laurence Museru akizungumza kwenye Mkutano wa wataalamu wa kutoa huduma za dawa ya usingizi na ganzi iliyofanyikakwenye hoteli ya Peacock jijini Dar es salaam.Baadhi ya wataalamu wa kutoa huduma za dawa ya usingizi na ganzi wakiwa kwenye mkutano uliofanyika katika hoteli ya Peacock jijini Dar es salaam.(Picha na Emmanuel Massaka wa Michuzi Tv)Muonekano wa viifaa tiba vinavyotumiwa na wataalamu wa kutoa huduma za dawa ya usingizi na ganzi.Wataalam hao wakiwa katikapicha ya pamoja mara baada ya ufunguzi rasmi wa mkutano huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...