Na.Khadija seif,Globu ya jamii
MALKIA
wa muziki wa Afro Pop nchini Mwanahawa Abdul a.k.a Queen Darlin ameiona
nyota ya jaha kupitia muziki wa Diamond kufika mbali kisa Mwanadada Tanasha.
Darlin
amesema Tanasha anafanya muziki, na soko lake amelenga mbali sio Afrika
Mashariki tu kutokana na kujuana na watu mbalimbali ambao alikuwa akifanya
nao kazi kama video vixen .
"Kuwepo
lebo ya wasafi classic baby (WCB) ambayo anasimamia kaka yangu diamond
hamaanishi kuwa natoa ngoma nikijisikia au ninavopenda mwenyewe, bali ni
kanuni na taratibu ambazo zimewekwa kwa kila msanii kutoa wimbo kwa wakati
sahihi kulingana na soko linahitaji kitu gani "
Darlin ambaye amekuwa na muonekano wa kimanjonjo awapo jukwaani,amewashukuru mashabiki wake ambao wameupokea vizuri wimbo wake mpya "muhogo"
unaofanya vizuri vituo mbalimbali na kujiongezea wigo wa mashabiki kila kona ndani na nje ya nchi,wakiwemo Wanaume kutokana na taswira inayojengeka kwenye wimbo huo.
"Muhogo
ni wimbo ambao ulipita BASATAa na kupewa vibali vyote kutokana na
wimbo huo kutumia tafisida na kuficha maana halisi, na ndio
kitu pekee ambacho hata wimbo wa nyegezi uliotungwa na Rayvan aliomshirikisha Diamond ulifungiwa kutokana na kutokuwepo kwa tafisida kwa baadhi ya
matamshi na kuleta ukakasi kwa hadhira, hivyo nilitumia nafasi hiyo
katika kutengeneza na kuboresha wimbo wangu,"
Mwanadada huyo ambaye ameonaka kuendelea kutikia anga ya muziki wa Bongofleva kwa upande wa wasanii wa kike,Darlin amebainisha wazi kuwa bado anamkumbuka sana Alikiba katika kushirikiana nae
kwenye kazi zake kimuziki na kutengeneza wimbo kama wajua nakupenda
uliofanya vizuri miaka ya 2009.
"Alikiba akitoa ngoma mpya naingia Youtube natazama kama nzuri nasifia, kama mbaya naweka wazi sisi ni watu wa karibu sana "
Darlin amewaomba
mashabiki wake waendelee kumuunga mkono kwenye kazi zake na wiki hii
anatarajia kutoa ngoma mpya mbili,moja itakayoitwa 'tawire' na 'mbali'aliomshirikisha msanii mwenza wa kundi la WCB .
Mwanahawa Abdul a.k.a Queen Darlin
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...