Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto) akisalimiana na Watumishi wa Ofisi kuu ya wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Mpwapwa alipowatembelea leo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma. Kushoto ni Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dkt. Jacob Chimeledya
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akipatiwa zawadi ya Biblia na Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dkt. Jacob Chimeledya alipomtembelea leo katika Ofisi kuu ya wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Mpwapwa Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (katikati) akipatiwa zawadi ya Mbuzi wawili na Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dkt. Jacob Chimeledya alipomtembelea leo nyumbani kwake Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma. Kushoto ni Mke wa Askofu ambae ni Mshauri wa Wanawake ndani ya Dayosisi katika Malezi ya Kikristo, Ndg. Mwezwa Chimeledya
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto) akipatiwa maelezo na Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Queen Esther, Mwl. Angelina Kashangaki (kushoto) alipoitembelea Shule hiyo inayomilika na kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Mpwapwa Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma. Kulia ni Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dkt. Jacob Chimeledya
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kulia) akikagua darasa la Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Queen Esther wakati alipoitembelea Shule hiyo inayomilikiwa na kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Mpwapwa iliyopo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma. Wa pili kushoto ni Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dkt. Jacob Chimeledya na Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Mwl. Angelina Kashangaki
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akikagua ujenzi wa darasa la Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Queen Esther wakati alipoitembelea Shule hiyo inayomilikiwa na kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Mpwapwa iliyopo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma. Kulia ni Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dkt. Jacob Chimeledya
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Queen Esther wakati alipoitembelea Shule hiyo inayomilikiwa na kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Mpwapwa iliyopo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.
 Wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Queen Esther wakimsikiliza Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (hayupo kwenye picha) akizungumza wakati alipoitembelea Shule hiyo inayomilikiwa na kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Mpwapwa iliyopo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai akizungumza na wanafunzi wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Queen Esther wakati alipoitembelea Shule hiyo inayomilikiwa na kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Mpwapwa iliyopo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma. Kuanzia kushoto ni Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dkt. Jacob Chimeledya, Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Queen Esther, Mwl. Angelina Kashangaki na Katibu wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Mpwapwa, Ndg. Charles Makuyu
 Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (kushoto) akimpatia zawadi ya vitabu Mkuu wa Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Queen Esther, Mwl. Angelina Kashangaki wakati alipoitembelea Shule hiyo inayomilika na kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Mpwapwa Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma.

Spika wa Bunge, Mhe. Job Ndugai (wa pili kushoto waliokaa) akiwa katika picha ya pamoja na wanafunzi wa kidato cha nne (4) Shule ya Sekondari ya Wasichana ya Queen Esther wakati alipoitembelea Shule hiyo inayomilikiwa na kanisa la Anglikana Tanzania Dayosisi ya Mpwapwa iliyopo Wilayani Mpwapwa Mkoani Dodoma. Kuanzia kushoto waliokaa ni Askofu Mkuu Mstaafu wa Kanisa la Anglikana Tanzania, Dkt. Jacob Chimeledya, Mwalimu Mkuu wa Shule hiyo, Mwl. Angelina Kashangaki  na Katibu wa kanisa la Anglikana Dayosisi ya Mpwapwa, Ndg. Charles Makuyu

(PICHA NA OFISI YA BUNGE)

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...