Na Ripota Wetu

WAZIRI wa Ulinzi nchini Uturuki Hulusi Akar amesema nchi yake inajiandaa kwa vikwazo vya Marekani baada ya kuendelea na mpango wake wa kununua mfumo wa kujilinda na makombora kutoka Urusi.

Katika taarifa iliyosambazwa jana Jumatano, Akar amesema wametuma watu wake nchini Urusi kupewa mafunzo ya kutumia mfumo huo wa S-400, yatakayoanza siku chache zijazo na kuendelea kwa miezi kadhaa.

Inadaiwa kuwa Ikulu ya White House ilitishia kuiwekea vikwazo Uturuki, chini ya sheria ya vikwazo inayozuia shughuli za kibiashara na sekta ya intelijensia na ulinzi ya Urusi.

Hata hivyo Marekani, inataraji kuiongezea mbinyo Uturuki, ambayo ni mshirika wa Jumuiya ya Kujihami ya NATO ili kununua mfumo wa Marekani, lakini Uturuki imekataa kuachana na ununuzi wa mfumo huo wa Urusi.

CHANZO -DW SWAHILI

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...