NCHI za Umoja wa Ulaya zimeahidi kuendelea kusimama pamoja wakati wote ili kuwa taasisi yenye nguvu kubwa duniani baada ya kushuhudia miaka mingi ya migawanyiko ya ndani ikitokea. 

Haya yameelezwa kwenye mkutano ambao haukuwa rasmi,uliowakutanisha viongozi 27 ambao ni wanachama wa umoja huo waliokutana katika Mji wa Sibiu ,Romania. 

Akizungumza katika mkutano huo, Kansela wa Ujerumani Angela Merkel amesema ulimwengu haulali na kwa hiyo lazima wawe wabunifu, wawe imara na wawe na umoja. 

Na kwamba mpango wa Uingereza kujiondoa katika Umoja huo umeigubika jumuiya hiyo kwa zaidi ya miaka miwili, kwa hivyo mkutano wa jana ulikuwa fursa nzuri ya kutoa mwito wa umoja na kusisitiza kuhusu kanuni za misingi za Umoja wa Ulaya. 

Uingereza bado kimsingi ni mwanachama wa Umoja wa Ulaya lakini Waziri Mkuu Theresa May hakuhudhuria mkutano huo wa kilele wa Romania na akabaki London kujaribu kuupigia debe mpango wake wa Brexit upitishwe bungeni. 

CHANZO DW .

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...