Daktari wa macho wa Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila Geofrey Josephat
akitumia kifaa maalum kumfanyia uchunguzi mtoto sehemu ya nyuma ya jicho ili
kubaini kama ana tatizo. Hospitali ya Mloganzila imefanya zoezi la uchunguzi wa macho bure kwa watoto wenye umri chini ya
miaka mitano ikiwa ni maadhimisho ya wiki ya saratani ya jicho kwa watoto (Retinoblastoma).
Mtaalam wa miwani Nestory
Massawe akimpima uwezo wa kuona mbali mtoto Shamsa Mbegu.
Daktari Bingwa wa macho
Suzan Mosenene (kulia) akimfanyia uchunguzi wa macho mtoto, huduma ya uchunguzi
wa macho bure kwa watoto imefanyika Mei 16 hadi Mei 17, 2019.
Baadhi ya wazazi ambao
wamewaleta watoto wao katika Hospitali ya Mloganzila kwa ajili ya kufanyiwa
uchunguzi wa macho.
Hospitali ya Taifa Muhimbili-Mloganzila imefanya zoezi la uchunguzi wa
macho bure kwa watoto wenye umri chini ya miaka mitano ikiwa ni maadhimisho ya wiki
ya saratani ya jicho kwa watoto (Retinoblastoma).
Katika zoezi hilo ambalo limefanyika Mei 16 hadi Mei 17, 2019 zaidi ya
watoto 100 wamehudumiwa ambapo baadhi yao wamekutwa na matatizo ya uoni hafifu,
mzio na kovu kwenye macho.
Daktari Bingwa wa macho kutoka Muhimbili Judith Mwende amesema ugonjwa wa
saratani ya jicho kwa watoto ni hatari na husababisha upofu na kifo endapo usipotibiwa
mapema na wakati mwingine hulazimu kuliondoa jicho ili kuokoa maisha ya mtoto.
Akifafanua Dkt. Mwende amesema takwimu za miaka mitatu za kutibu na kufuatilia ugonjwa wa saratani ya
jicho kwa watoto katika Hospitali ya
Taifa Muhimbili (MNH) takribani asilimia 60-70 ya watoto hao huwa wako kwenye
hatua mbaya za ugonjwa.
Hali hiyo husababisha asilimia 50-60 kupoteza maisha kwa sababu ya
kuchelewa kufika kupata huduma inayostahili na kwa wakati.
Ametaja sababu za kucheleweshwa hospitalini
ni familia kutokufahamu dalili za
ugonjwa na hatari zake, wahudumu
wa afya ya msingi kuchelewesha rufaa kwa kutofahamu dalili za ugonjwa, familia
kukosa nauli kufuata matibabu pindi wakipewa rufaa , familia kutafuta matibabu
mbadala mpaka wakiona hatua za mwisho za ugonjwa na kukataa mapendekezo ya
wataalam hasa kuliondoa jicho pale inapohitajika ili kunusuru maisha ya mtoto
Dalili za mwanzoni za saratani ya jicho kwa watoto ni weupe
kwenye mboni ya jicho ambao unaonekana kirahisi kwenye giza au mtoto akipigwa picha
na flush, kengeza, jicho kuvilia damu kuwa jekundu, kubadilika rangi au kuuma.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...