Na Karama Kenyunko, Globu ya Jamii.
MAHAKAMA ya Hakimu Mkazi Kisutu imeamuru msanii wa Filamu nchini, Wema Sepetu kumkamatwa kwa kuruka dhamana.Wema anashtakiwa mahakamani hapo na kesi ya kusambaza video ya ngono katika mitandao ya kijamii kupitia simu yake ya kiganjani.
Mahakama imeto hati hiyo ya kumkamatwa Wema, leo Juni 11,2019 mbele ya Hakimu Mkazi, Maira Kasonda, baada ya upande wa mashtaka ukiongozwa na Wakili wa Serikali, Silvia Mitanto kudai kwamba mshtakiwa hayuko mahakamani na hakuwa na taarifa yoyote.
Hata hivyo utetezi uliotokewa na wakili wa Wema, utetezi, Ruben Simwanza, ambae amedai mshtakiwa alifika Mahakamani lakini ameugua ghafla na hivyo ameshindwa kuingia katika chumba cha Mahakama, haukuweza kumsaidia Wema, na hivyo amri ya yeye kukamatwa ikatolewa.
Akitoa uamuzi huo, jakimu Kasonde amesema Mahakama inatoa hati ya kumkamata mshtakiwa kwa sababu kama alifika alishindwa nini kuingia mahakamani.
Katika kesi hiyo, Wema anakabiliwa na shtaka moja la kuchapisha video ya ngono katika mtandao wa kijamii, kosa analodaiwa kutenda kati ya Oktoba 15, 2018 katika maeneo mbalimbali ya Jiji la Dar Es Salaam, ambapo anadaiwq kusambaza video za ngono kupitia akaunti yake ya Instagram, picha ambazo inadaiwa kuwa haina maudhuil.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...