Shirikisho la soka Tanzania (TFF) limemfuta kazi mkurugenzi wa Ufundi wa shirikisho hilo Ammy Ninje  kutokana na sababu mbalimbali za kifamilia na kimasomo. 

Pia TFF imelivunja bechi lote la ufundi la Serengeti Boys ambalo lilikuwa chini ya Kocha Oscar Milambo na nafasi hizo zitajazwa hapo baadae.

Afisa habari na Mawasiliano wa TFF Clifford Ndimbo amesema,Ninje hajafukuzwa ila matatizo na majukumu ya kifamilia yamefanya Tff wachukue maamuzi hayo ila ataendelea kutumika katika masuala mbalimbali ya kisoka.

  "Sio kwamba tumemfukuza Kutokana na masuala ya kifamilia Mkurugenzi wa Ufundi wa TFF, Ammy Ninje bali Rais Wallace Karia amesema kutokana na masuala ya kifamilia yanayomtinga basi atarudi Uingereza lakini tutaendelea kumtumia katika masuala ya soka na atakayeshika nafasi yake tutamtangaza hivi karibuni. Kwa upande wa Benchi la ufundi pia ni kweli tumelivunja na tutatangaza hapo baadaye pia benchi jipya la ufundi," amesema Ndimbo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...