Na.Khadija seif,Globu ya jamii

*Washiriki wapewa fursa kushiriki mashindano ya keki juni 26

Tamasha la waokaji  kufanyika rasmi jijini Dar es salaam.

Akizungumza wakati wa kukabidhi zawadi kwa washindi ambao walijitokeza kwenye tamasha hilo Muandaaji Laura Mkula amesema imekua ni mara ya kwanza kuandaa shindano hilo na muitikio umekua mkubwa kiasi chake kuanzia mchakato wa fomu hadi kushiriki kikamilifu.

" Imekua ni fursa ya kipekee kwa wajasiriamali wakubwa kwa wadogo hasa waokaji wa vitafunwa kushindanishwa na kupata ujuzi mpya kuboresha biashara zao,"

Aidha,Mkula ametoa ushauri kwa washiriki wote kuboresha biashara zao huku swala la kujitangaza likipewa kipaumbele na kutengeneza mitandao ya kijamii Kama njia pekee ya kuwasiliana na wateja wao na kuwafikia kwa haraka zaidi.

"Mitandao ya kijamii ifanye biashara yako ya kwanza ili iweze kukupatia wateja wengi zaidi na kupika vitu mbali mbali kutokana na idadi ya wateja wako,"

Pia amepongeza washiriki wote ambao wameweza kujitokeza kwenye tamasha hilo kwani wote ni washindi na wamefanya uthubutu wa kushiriki japo washindi ni watatu ambao wameweza kushinda zawadi.

"Waliochukua fomu walikua 15 lakini tumeweza kupata washindi watatu , Diana bakery ambae mshindi wa kwanza aliyejishindia jiko la kuoka keki ,hakim Bakery, huku mshindi wa pili fatna production alipewa vifaa vya upishi pamoja na jastin makeki ambae alifanikiwa kuibuka mshindi wa tatu alizawadiwa vifaa vya upishi wa keki,"

Kwa upande wake mshindi wa kwanza edina cake amepongeza washiriki wote pamoja na muandaaji wa shindano hilo huku akiwataka wakina kuacha kujibweteka nakusubiri kuajiriwa.

"Kwa mara ya kwanza nilitamani kushiriki shindano hilo na Leo nimeibuka mshindi japo kuna wakati nilikata tamaa nakuona ni vitu vya ubabaishaji ,"
Aidha, jaji wa tamasha hilo Alexander vitalis amewahimiza washiriki wote kuchukua ujuzi zaidi ili kushiriki mashindano makubwa zaidi.

"Wote wamefanya vizuri japo hakuna vitu ambavyo vimekua tofauti sana kuanzia ladha na baadhi ya mionekano ya keki,"

Pia vitalis ametoa nafasi ya upendeleo kwa washiriki wote kushiriki shindano la keki bure linaloandaliwa na zena Sharif (Anezliytta) juni 26 mwaka katika ukumbi wa kingsolomon jijini Dar es salaam .
Majaji wakipita kila meza ya mshiriki kuonja keki kwenye tamasha la waokaji lilofanyika katika ukumbi wa little threate jijini Dar es salaam 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...