Na Khadija seif,Globu ya jamii

JUMLA ya warembo 15 wamefanikiwa kuingia kwenye kinyang'anyiro cha kumsaka miss Tanga mwaka huu,2019.

Akizungumza na waandishi wa habari  jijini Tanga muandaaji wa shindano hilo Chuchu Hansy amesema warembo walijitokeza wengi kiasi kwamba wote ni wazuri na wana vigezo vya kuingia kambini.

"Warembo  mkoa wa Tanga wamejitokeza wengi kiasi imekua ngumi kwa majaji kuchagua yupi anastaili kuingia kwenye kinyang'anyiro hiki lakini tumeweza kutoa nafasi ya upendeleo na kuongeza baadhi ya washiriki na hatimae idadi kufikia 15,"

Hata hivyo Chuchu amewataka warembo watakapoingia kambini kuwa na nidhamu ya hali ya juu kuanzia kwa viongozi wao wakiwa Kama walezi wao na kwa warembo watakaoonyesha utovu wa nidhamu hatuwaonea huruma kuwaondoa.

"Sitosita kumuondoa mrembo yoyote atakaye kuwa hana nidhamu,hata Kama atakuwa ni mrembo mzuri na mwenye vigezo vyote kuanzia elimu,figa ,rangi na kipaji,"alisisitiza Chuchu.

Amesema kwa sasa sasa warembo wanatarajia kuingia kambini julai 1 mwaka huu .


Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...