Na Said Mwishehe,Globu ya jamii
WIZARA ya Fedha na Mipango
imewataka wadaiwa sugu wa madeni ya Commodity Import Suport (CIS) na
Na Food Aid Counterpart Fund (FAFC) wakiwemo wafanyabishara maarufu nchini
Yusuph Manji na Mohamed Dewji 'MO' kuhakikisha wanalipa madeni hayo mara
moja.
Taarifa iliyotolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Fedha na
Mipango Bw. Dotto James katika tangazo la wadaiwa hao iliyotolewa leo Juni 19, 2019
kwa vyombo vya habari jijini Dar es Salaam imeeleza kuwa Wizara ya Fedha
na Mipango inawataka wadaiwa sugu wa madeni hayo kuhakikisha wanalipa
mara moja na kwamba licha ya kutolewa tangazo la awali bado wameshindwa
kuitikia mwito.
"Madeni haya ni mkopo wenye masharti nafuu
yaliyotolewa kwa Taasisi, Kampuni, Viwanda na Wafanyabiashara, ambapo
wakopaji walitakiwa kulipa deni bila kutozwa riba katika kipindi cha
Miezi 18 tangu walipopewa mikopo hiyo.
"Kwa mujibu wa sheria ya
CIS (The Commodity Import Support Regulation Act, CAP 261 R. E. 2002
(s.8 (1)(b), Mkopaji akichelewa kulipa katika kipindi cha miezi 18 tangu
kupatiwa mkopo, atapaswa kulipa riba ya asimilia sawa na kiwango
kinachotozwa na Benki Kuu ya Tanzania inapoikopesha Serikali katika
kipindi husika. Zaidi ya makampuni 980 yalikopeshwa chini ya utaratibu
huu,"amesema James kwenye taarifa hiyo.
Kwa mujibu wa Wizara
hiyo, Wizara hiyo imesema kuwa Serikali inatangaza kwa mara ya mwisho
kutokana na baadhi ya wadaiwa ambao wameshindwa kuitikia mwito wa
matangazo ya awali ya Desemba 30 mwaka 2015 na Aprili 5 mwaka 2018.
"Hatua za kisheria zitachukuliwa mara baada ya kutoka kwa tangazo hili,"amesema.
"Hatua za kisheria zitachukuliwa mara baada ya kutoka kwa tangazo hili,"amesema.
Katika orodha ya kwanza ya wadaiwa sugu wa
madeni yatokanayo na mkopo huo ni Yusuph Manji aliyekopa kupitia kampuni
zake za Farm Equipment Tanzania Ltd, Quality Group Ltd, Dunhill
Motors Ltd, Quality Seed Ltd na Quality Garage Ltd na Mohamed Dewji
kupitia 21st Century Textiles Ltd na Afritex Ltd
Mdaiwa
mwingine ni S. S Rashid kupitia Pwani Tours and Safari Ltd na Pwani
Investment Ltd. Pia Issack Bugali kupitia Dar es Salaam International
School Trust Fund na Upoloto Farm Ltd.Pia yumo K.B Medicare Ltd (Prof.
Bernard Kirei), Siza Cold Storage Co.Ltd (Stephen Wasira)
8. Sorority Co. Ltd (Martha Lyimo) 21st Century, Afritex Ltd,na Kichonge Miller (Bokeye Kangoye)
Wadaiwa
sugu wengine ni Rela Investment Company Ltd (Ahiya E. Lukumayi), Bahari
Motor Co Ltd (Hashim Rungwe), Andrew Traders Co Ltd (Andrew Richard
Kisenge), Oth Investment Co Ltd (Boniventure Boniventure)
na Kiomboi Kisiriri Pharmacy Ltd (Dkt Kingu)
Wizara
hiyo imesema kwa maelezo zaidi imewataka wadaiwa hao kuwasiliana na
Kikosi Kazi, Wizara ya Fedha na Mipango, Dar es Salaam, chumba Na. 352,
Simu Na. +255 739403025/ 2122282285
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...