Balozi wa Uingereza nchini Tanzania amefanya ziara ya siku moja Hospitali ya Taifa Muhimbili (MNH) ambako amekagua vifaatiba vikiwamo vinavyotumika kutoa huduma kwa wagonjwa wa macho. Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Cooke akiuliza jambo kuhusu matumizi ya Optical Coherence Tomography (OCT) inavyotumika kutambua magonjwa yaliopo kwenye pazia la macho (retina) kutoka kwa Dkt. Moin Mohamed wa Hospitali ya Mtakatifu Thomas nchini Uingereza. Kushoto ni Mkurugenzi wa Huduma za Upasuaji wa MNH, Dkt. Sufiani Baruani wa MNH. Jana Shule ya Kwaya ya Westminister Cathedral ya nchini Uingereza kupitia Hospitali ya Mtakatifu Thomas iliyopo nchini humo ilitoa mashine ya OCT ili kusaidia wagonjwa wenye matatizo ya macho nchini. 
Moja ya mashine inayotumika kutoa huduma ya magonjwa ya macho. 
Balozi wa Uingereza nchini Tanzania, Sarah Cooke aha akiwa katika picha ya pamoja na wataalam wa magonjwa ya macho wa MNH.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...