Benki ya CBA ikishirikiana na kampuni ya Vodacom imefanya droo yake ya 5 ya kuadhimisha miaka 5 ya huduma ya MPawa yenye lengo la kuongeza ushirikishwaji wa kifedha kwa wateja wake kwenye makao makuu ya benki hiyo jijini Dar es salaam.

Katika kusherehekea maadhimisho hayo, promosheni hiyo inajumuisha droo za kila wiki zilizohusu kuwekeza na kukopa na MPawa huku ukitoa washindi zaidi ya 340 walioibuka na mara mbili ya akiba zao kuanzia kiwango cha Tsh 1000-200,000, simu janja na muda wa maongezi.

Katika kuongelea kuhusu huduma hii ya MPawa, Meneja Masoko wa benki hiyo Bw Solomon Kawiche aligusia mambo 3 muhimu kwenye maadhimisho hayo ya Miaka 5.

M-Pawa inasherehekea miaka 5, ni mafanikio gani yameonekana tangu kuanzishwa kwa huduma hii? Mpawa ilianza na wateja 4 tu ila hadi leo hii imefikisha wateja Mil 8.5 na imefanikiwa kurahisisha Maisha ya wananchi wengi ambao wapo mbali na huduma za kibenki kwa kuwapatia huduma nafuu za kibenki ikiwemo kukopa kiasi kidogo cha hadi 1000 ambacho hauwezi kupata kupitia huduma za benki.

M-Pawa imefanikiwa kutoa huduma ya kuhifadhi akiba kwa kiwango cha chini cha hadi Tsh 1, hakuna benki nyingine ndani ya Tanzania inayotoa huduma kama hii na kurahisisha huduma za kibenki bila ya kuwa na utaratibu mrefu kukamilisha miamala. Watumiaji wa M-Pawa hawana haja ya kutembelea matawi yetu na kupitia huduma hii, wateja wetu wanapata faida kupitia akiba zao.

Akiba za wateja wa MPawa pia zipo kwenye usalama wa hali ya juu kwasababu hakuna makato au gharama zilizofichika. MPawa imeinua hali ya Maisha ya mamilioni ya watanzania hususani wafanyabiashara wadogo na bila kusahau kuwa imekuwa ikitoa uhakika wa kifedha wakati wa dharura; mteja anaweza kukopa muda wowote na wakati wowote ule.

Nini malengo ya baadae ya M-Pawa? Ikiwa ni huduma ya kwanza ya kidigitali Tanzania, MPawa itaendelea kugusa miasha ya wananchi wengi ambao wapo mbali na huduma za kibenki na itaendelea kujidhatiti kwenye kuwajumuisha kifedha wateja wake. Kama benki, tuna maleno ya kuwekeza zaidi kwenye huduma hii kuhakikisha kuwa inaendana na maendeleo ya sasa ya kisayansi na Teknolojia na kuwezesha huduma hii kwenye application. Nini maoni yako kwenye huduma za kifedha za kiditali hususani M-Pawa?

Huduma za kifedha za kidigitali kwenye dunia ya leo ni sio kitu ya kupuuza hususani huduma kama MPawa kwa sababu ya urahisi wake kwenye gharama, uaminifu wake na urahisi wake katika kuitumia. MPawa inapatika kupitia simu yoyote ya mkononi, ni huduma ya kibenki iliyorahisishwa kutumia mahali popote kwa gharama nafuu na humpatia mteja faida kupitia akiba anayoweka bila kuwa na gharama zilizofichwa. Hili linaupa upekee huduma hii ya M-Pawa

Mshindi mkubwa wa maadhimisho haya ya Miaka 5 ya MPawa ataibuka na zawadi ya Million 15 za kitanzania kwenye droo ya mwisho ya promosheni hiyo. Kwa maelezo zaidi kuhusu huduma hii, wateja wanaweza kutembelea mitandao ya kijamii ya benki ya CBA/Vodacom au kutembelea menyu ya MPawa kwa kubonyeza *150*00# kupitia mtandao wa simu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...