Wananchi wakichota maji katika kituo cha kuchotea maji cha Mradi wa Maji Hedaru katika eneo la Hedaru B, wilayani Same mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akiwa katika eneo lilipojengwa chanzo cha Mradi wa Maji Hedaru katika Kijiji cha Gundusine, Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akiwasikiliza wakazi wa Kijiji cha Gundusine katika Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akikagua moja ya kituo cha kuchotea maji cha Mradi wa Maji Hedaru katika mji wa Hedaru, Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro.
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso akiongozana na Mkuu wa Wilaya ya Same, Rosemary Senyamule wakati wakikagua Mradi wa Maji katika Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro.
Tenki jipya la kuhifadhi maji la Mradi wa Maji Hedaru, wilayani Same, mkoani Kilimanjaro.
……………………..
Naibu Waziri wa Maji, Mhe. Jumaa Aweso (Mb) amekagua Mradi wa Maji Hedaru uliogahrimu Shilingi bilioni 1.7 kwenye Mji wa Hedaru kwa lengo la kujionea changamoto zinazoukabili, ikiwemo usimamizi wa mradi katika Wilaya ya Same, mkoani Kilimanjaro.

Naibu Waziri Aweso amekagua vituo vyote vya maji vilivyojengwa kwa lengo la kutoa huduma kwa wananchi katika mradi huo na kukuta vyote vikitoa maji, lakini akabaini mambo yafuatayo:- 

Chanzo cha maji kutokuwa na uwezo wa kukidhi mahitaji ya wananchi. 
Matumizi ya mfumo wa nishati ya jua baadala ya nishati ya umeme ambayo imefika kwenye mji huo. Usimamizi mbovu wa Kamati za Maji uliosababisha mradi kutojiendesha kwa faida. 

Mgawanyo wa maji usio na uwiano sahihi na kusababisha mgogoro kwa wananchi. 

Mara baada ya kukagua mradi huo, Naibu Waziri Aweso ameitaka Mamlaka ya Majisafi na Usafi wa Mazingira Moshi (MUWSA) kusimamia mradi huo katika kipindi cha mpito mpaka watakapo patikana viongozi wa kamati mpya itakayosimamia mradi.Pili, ameelekeza yafanyike mabadiliko ya mfumo wa nishati ya jua kwenda kwenye umeme.

Tatu, ameelekeza kitafutwe chanzo kipya cha uhakika kitakachokidhi mahitaji halisi ya wananchi.Nne, amewataka wataalam kutoka Bonde la Mto Pangani kufika na kutatua changamoto ya watumiaji maji.Tano, amesisitiza ushirikishwaji na elimu itolewe kwa wananchi katika uendeshaji wa mradi ili waweze kuwajibika katika maendeleo ya mradi.

Aidha, Naibu Waziri Aweso amesema kuna umuhimu mkubwa wa kuwashirikisha wananchi katika hatua zote za ujenzi wa miradi yote ya maji, waweze kuwa wasimamizi wazuri wa miradi itakayokuwa endelevu.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...