Wakati Mamlaka ya Mawasiliano Tanzaia (TCRA) inaendela na utekelezaji wa zoezi la usajili wa laini za simu kwa njia ya biometria, TCRA imebaini kuwa kuna watu wanaojihusisha na usajili wa SIMU bila kuidhinishwa na watoa huduma za mawasiliano.
Kwa mujibu wa kifungu cha 92 na 97 cha Sheria ya Mawasiliano ya Kielektroniki na Posta, 2010 na Kanuni ya 9,10, na 11 ya Kanuni za Usajili wa Laini za Simu (Sim Card Registration Regulations, 2018), TCRA inapenda kuutaarifu na kuukumbusha Umma kuwa:-
-
Ni marufuku kwa mtu yeyote kuuza, kusambaza au kusajili laini za simu bila kuwa na uthibitisho kuwa ameidhinishwa na mtoa huduma za mawasiliano kutoa huduma hizo;
-
Yeyote anayejihususha na uuzaji, usambazaji au usajili wa laini za simu anatakiwa kuwa na ofisi ya kutolea huduma hiyo ya usajili wa laini za simu; na
-
Ni kosa la jinai kwa mtu yeyoye kuuza, kusambaza au kusajili laini za simu bila
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...