Na Woinde Shizza Michuzi Tv ,Arusha

Wanafunzi wa kidato cha nne kutoka shule mbali mbali jijini Arusha wamepongeza chuo cha uhasibu kwa kuandaa tamasha ambalo limewafanya kuweza kuongeza ujuzi waliokuwa hawana awali.

Wakizungumza kwa nyakati tofauti wakati wa maonyesho ya Taaluma kwanye chuo cha uhasibu wanafunzi hao wamepata fursa ya kujifunza mambo mbali mbali ikiwemo kutambua na kuwa na uwelewa kuchagua kozi zitakazo wafaa katika elimu ya juu .

Wamesema kwamba maonyesho hayo yamewatengenezea uzoefu na ujuzi kwani wamekutana na wananchuo wanao soma fani mbali mbali hivyo wanataraji kujiunga nazo mara baada ya kidato cha nne na hiyo imewapa hamasa ya kufikia elimu ya juu

Baadhi ya wanachuo wa chuo cha uhasibu wanaoshiriki maonyesho hayo wanaelezea Faida ya maonesho hayo ni kujitangaza kwa jamii kutambua masomo mbali mbali yanayo tolewa kwa wanafunzi na jinsi gani yanawasaidia kujiajiri nwenyewe

moja wa wakufunzi chuoni bundalla bachia hapo katika maonyesho hayo ameleza kwamba kumekua na mwitikio mkubwa kwa wanafunzi wa secondary kutembelea mabanda na kujifunza mambo mbali mbali kutoka kwao

Akitembelea tamasha hilo waziri wa elimu na mafunzo ya Amali serikali ya mapinduzi ya Zanzibari Riziki Pembe Juma alisema ni fursa nzuri maana wanafunzi wanatumia zaidi katika tamasha hili kufanya mafunzo ya vitendo.

Alisema kuwa matamasha haya yatasaidia wanafunzi hawa kwani watabadilishana uzoefu wa aina mbalimbali ,pamoja na ujuzi wa aina mbalimbali ,pia maonyesho hayanasaidia wanafunzi hawa kupata muda wa kuonyesha kile ambacho wanajifunza hivyo ni jambo jema sana chuo hichi wamefanya.

Kwa vile ni mara ya kwanza kufanya basi waendelee kufanya mara kwa mara na wasishirikishe shule za serikali tu bali washirikishe na shule za binafsi uli wabadilishane uzoefu,lengo letu la serikali ni kuona vijana wetu wanajifunza na kujiajiri hapo baadae"alisema Riziki

Alitoa wito kwa vyuo vingine kuiga mfumo huu kwani ni mzuri unasaidia wanafunzi kujifunza mambo mbalimbali.
mmoja ya mwanafunzi wa shule ya sekondari ya Arusha bundalla bachia akiongea na waandishi wa habari juu ya faida za tamasha hilo 
Daktari kutoka hospitali ya NIC akimpima mmoja wa wanafunzi aliuzuria katika tamasha hilo ambapo hospitali ya nic imetoa huduma ya upimaji sukari na presha .
Waziri wa elimu na mafunzo ya Amali serikali ya mapinduzi ya Zanzibari Riziki Pembe Juma wa pili kulia akiangalia baadhi ya vitu vinalivyoletwa na wanafunzi katika maonyesho yaliondaliwa na wanavyuo yanayofanyika ndani ya viwanja vya chuo cha uhasibu Arusha

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...