Na Humphrey Shao, Michuzi Tv Dar es Salaam
Wadau was sekta ya Maziwa nchini wamekutana jijini Dar es Salaam leo kujadili na kupitia sheria ya Maziwa sura 262 ya mwaka 2004 na kanuni zake.
Akizungumza wakati wa kufungua mkutano huo Kaimu Msajili wa bodi ya Maziwa nchini, Dkt. Sophia Mlote Amesema sheria Ina miaka 15 tangu ianze kutumika mwaka 2004 na kanuni zake ni za mwaka 2007 na 2012.
Amesema Tasnia ya Maziwa imekua na mabadiliko mbalimbali na mambo mengi yamejitokeza ambayo ni ya msingi katika uendelezaji wa Tasnia ya Maziwa ambayo yanahitaji usimamizi wa kisheria.
" Kwa kutekeleza lengo la mkutano huu la kupitia sheria na kanuni zake kikamilifu na kutoa michango yetu tutaweza kuboresha usimamizi wa tasnia ya Maziwa ili kuiwezesha kusimamiwa ipasavyo" Amesema
Ametaja kuwa maeneo yatakayopitiwa na marekebisho haya ni sheria ya Maziwa Na.8 Sura 262 ya mwaka 2004 , kanuni ya uuzaji wa Maziwa na bidhaa zake nje na ndani ya Nchi ya mwaka 2012,usimamiaji wa madaraja ya Maziwa ghafi ya mwaka 2007.
Amesema kanuni ya usafirishaji wa Maziwa ghafi nayo inapitiwa,kanuni ya majukumu na kazi A wakaguzi ya mwaka 2007.
Alimaliza kwa kwa kusema majukumu ya bodi ya Maziwa kwa mujibu wa sura 262 ya mwaka 2004 ni kusimamia nankuendeleza uzalishaji ,usindikaji na uuzaji wa Maziwa.
Kaimu Msajili wa bodi ya Maziwa nchini,Dkt.Sophia Mlote akizungumza na wadau wa Maziwa nchini wakati wa mkutano Maalum was kufanya mapitio ya sheria ya Maziwa katika ukumbi wa Mvuvi House jijini Dar es Salaam.
Mwanasheria wa Wizara ya Mifugo na Uvuvi,Irine Lukindo akifafanua juu ya sherianya zamani na marekebisho yake kifungu kwa kifungu.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...