Na Humphrey Shao, Michuzi TV 

Waziri wa Viwanda na Biashara, Innocent Bashungwa Leo amefanya mazungumzo na wafanyabiashara wa kariakoo na kuhaidi kutatua kero sugu zinazozoletesha biashara katika soko Hilo.

Waziri Bashungwa amesema Wizara yake ipo tayari kushughulikia na kero hizo ikiwemo swala la tozo zisizo za lazima kwa wafanyabiashara na changamoto wanazokutana nazo kutoka kwa Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) na Bandari.

"Kwa hakika nimesikia kero zenu kwa hatua ya Kwanza nimezungumza na kamishna wa TRA ndugu yangu amekubali kufanya mkutano na nyie kesho saa nane pia katika mkutano huo atakuwepo kiongozi kutoka mamlaka ya Bandari nchini" Amesema Bashungwa.

Hata hivyo waziri Bashungwa aliwataka wafanyabiashara hao kulinda Viwanda vya ndani kwa kuuza bidhaa zinazopatikana hapa nchini kwani kwa kufanya hivyo wataweza kutekeleza sera ya Viwanda inayosimamiwa na Rais Magufuli.

Waziri Bashungwa aliwashukuru wafanyabiashara hao kwa kunitokeza na kuzungumza mambo ambayo yanahitaji lengo la kujenga uchumi wetu kwa kufanya Kariakoo kuwa Hub ya Afrika Mashariki.
 Waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa akionyesha kitabu Cha Blue Print ambacho kinaeleza namna serikali ya awamu ya tano imejipanga kuweka mazingira Bora ya kufanya biashara na uwekezaji.
 Wafanyabiashara waliofika katika ukumbi wa anatoglo kumsikiliza Waziri Bashungwa kama wanavyoonekana katika picha.
Washiriki wakimsikiliza kwa makini waziri wa Viwanda na Biashara Innocent Bashungwa katika mkutano wa wafanyabiashara.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...