Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati akifungua Mkutano mkuu wa mwaka wa dharura wa TCCIA mwaka 2019 uliofanyika New African Hotel Jijini Dar es salaam, leo tarehe 24 Agosti 2019. (Picha Zote Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo)
Sehemu ya washiriki wa Mkutano mkuu wa mwaka wa dharura wa TCCIA mwaka 2019 unaofanyika New African Hotel Jijini Dar es salaam wakifatilia hotuba ya waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, leo tarehe 24 Agosti 2019. 
Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) akisisitiza jambo wakati akifungua Mkutano mkuu wa mwaka wa dharura wa TCCIA mwaka 2019 uliofanyika New African Hotel Jijini Dar es salaam, leo tarehe 24 Agosti 2019. 
Sehemu ya washiriki wa Mkutano mkuu wa mwaka wa dharura wa TCCIA mwaka 2019 unaofanyika New African Hotel Jijini Dar es salaam wakifatilia hotuba ya waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) wakati wa ufunguzi wa mkutano huo, leo tarehe 24 Agosti 2019. 



Na Mathias Canal, Wizara ya Kilimo-Dar es salaam

Serikali imesema kuwa imejipanga lkuongeza ushirikiano na Sekta binafsi katika kuhakikisha kuwa kero na vikwazo vinaondolewa ili kuweka mazingira bora ya biashara na kuvutia uwekezaji wa ndani na nje ya nchi.

Waziri wa Kilimo Mhe Japhet Hasunga (Mb) ameyasema hayo leo tarehe 24 Agosti 2019 wakati akimuwakilisha Waziri Mkuu Mhe Kassim Majaliwa kufungua Mkutano mkuu wa mwaka wa dharura wa TCCIA mwaka 2019 huku akiongeza kuwa serikali imefanya uamuzi mahususi mwaka huu wa kuondoa muingiliano wa utoaji wa huduma za mashirika ya TBS na TFDA ili kupunguza usumbufu kwa Wanyabiashara. 

Alisema kuwa hizo ni hatua za awali na ametoa mwito kwa TCCIA kuhakikisha kuwa wafanyabiashara wanafuata sheria, kanuni na taratibu zote zilizowekwa ili kuondoa usumbufu wote unaoweza kujitokeza wakati wa kufanya biashara.

Alisema kuwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Mhe Dkt John Pombe Magufuli alizindua Mpango wa Pili wa Maendeleo ya Kilimo (ASDP II) tarehe 4 Juni, 2018. Kwa kutambua umuhimu wa Sekta Binafsi, moja ya maboresho makubwa ya ASDP II ukilinganisha na ASDP I ni kuipa nafasi kubwa zaidi Sekta Binafsi. 

Aliongeza kuwa ni wakati muafaka wa kubaini maeneo maalumu ambayo Taasisi hiyo ya TCCIA itaendelea kutoa mchango mkubwa katika kutekeleza programu hiyo ili iweze kufikia malengo yaliyowekwa.

Mhe Hasunga amesema kuwa ili kuhakikisha uboreshaji wa Mazingira ya biashara nchini, Serikali kwa kushirikiana na Sekta Binafsi iliandaa andiko maalumu “Blue Print” ambalo lilikwisha zinduliwa, pia mpango wa utekelezaji wake umeandaliwa na umeanza kutekelezwa. 

“Ni wajibu sasa wa kila pande yaani Sekta ya Umma na Binafsi kuhakikisha kuwa yale yote yaliyoainishwa katika andiko hilo yanatekelezwa ipasavyo” Alikaririwa Mhe Hasunga

Vile vile, amesema kuwa serikali imeendelea na jitihada za kuimarisha Mabaraza ya Biashara ya Mikoa na Wilaya ambapo tayari imeshaweka Mwongozo wa Mabaraza hayo ambayo TCCIA ni Sekretarieti. 

Waziri Hasunga amewataka washiriki hao kuchangamkia fursa zilizopo katika miradi mikubwa inayotekelezwa na Serikali nchini, hasa miundo mbinu ya reli ya Kisasa, mradi wa umeme wa bwawa la Nyerere, barabara za kisasa, bomba la mafuta, manunuzi ya ndege n.k. 

Alisema kuwa Fursa hizo kwa kupitia sera ya “Local Content” nao wakiwa wazawa wana nafasi kubwa ya kunufaika nazo. 

Amesema, Miradi hiyo ni mingi na itachukua muda mrefu ikitekelezwa kwa awamu tofauti. “Endapo kwa sababu moja au nyingine haukuweza kupata fursa ya kushiriki kazi kwenye mradi mmoja kwa sababu fulani zikiwemo sifa kadhaa basi, nakushauri ujipange vizuri kwenye miradi inayokuja, msikate tamaa” Alisisitiza Mhe Hasunga

Alisema kuwa serikali inatambua ushirikiano mzuri wa TCCIA na taasisi mbali mbali za Umoja wa Mataifa (UN) zikiwemo UNDP, UNIDO, FAO, UNV, UNESCO, ILO, na ITC, pamoja na Wadau wengine wa kimaendeleo kama Trade Mark East Africa. 

Ushirikiano huo kwa kupitia mifumo ya kielektroniki ya kuripoti na kufuatilia vikwazo mbalimbali (NTBs Reporting and Monitoring System) na utoaji wa vyeti vya Uasili wa Bidhaa kwa njia ya kielektroniki (Electronic Certificates of Origin) umesaidia sana uondoaji wa vikwazo vya biashara visivyokuwa vya kiforodha (NTBs). 

Pia, TCCIA imeshirikiana na Wadau wengine kama vile VSO, ENGEN, USAID, East African Trade Hub, BMZ, KOICA, JICA, TRIAS na DANIDA kupitia Local Investment Climate (LIC) kuimarisha biashara na mfumo wa majadiliano na sekta ya umma. Kwa kipekee ninawapongeza sana kwa mashirikiano hayo.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...