Na Said Mwishehe,Michuzi TV

WAKUU wa Nchi na Viongozi wa Serikali wa Jumuiya ya Maendeleo ya Nchi za Kusini mwa Afrika(SADC)wamepitisha kwa kauli moja lugha ya kuwa lugha rasmi ya nne itakayotumika kwenye jumuiya hiyo.

Kupitishwa kwa lugha hiyo kumetokana na Mwenyekiti mpya wa Jumuiya hiyo Rais Dk.John Magufuli kuomba lugha hiyo iingizwe kwenye jumuiya hiyo.

Akizungumza leo Agosti 18,2019 kwenye ufungaji wa Mkutano Mkuu wa 39 wa SADC ambao umefanyika ukumbi wa mikutano wa kimataifa wa Julius Nyerere Mwenyekiti huyo mpya ametoa taarifa ya kupitishwa kwa lugha ya Kiswahili kuwa rasmi.

"Nianze kutoa hotuba yangu ya kufunga mkutano wa 39 wa SADC kwa kueleza hapa,nilitoa ombi kuhusu lugha ya Kiswahili kutumika kwenye SADC.Wakuu wanachama wameiteua
lugha ya Kiswahili kuwa lugha rasmi ya  nne ya SADC.

"Narudia tena nawashukuru wakuu wa nchi na wakuu wa Serikali kwa kukubali lugha hiyo iwe rasmi kwenye jumuiya yetu.Baba wa Taifa amekuwa na heshima kubwa sana katika Bara la Afrika.Katika maisha wapo wanajitolea kwa mambo mbalimbali, wapo wanatoa figo,wapo wanaotoa fedha na utoaji wa aina nyingine," amesema.

Amefafanua Mwalim Julius Nyerere yeye aliamua kutoa upendo na maisha yake kwa ajili ya wengine na hivyo sehemu kubwa ya maisha aliyatumia kuhakikisha nchi za Afrika zinakuwa salama  na ndio maana nchini Tanzania kuna maeneo mbalimbali ambayo yalikuwa kambi za wapigania uhuru na hasa nchi za Kusini mwa Afrika.

" Mwalimu Nyerere alishiriki kwa vitendo kwa ajili ya kuhakikisha nchi za Afrika zinakuwa huru.Tanzania imekuwa na kambi nyingi za wapigania uhuru na mojawapo ilikuwa eneo la Kongwa ambako anatoka  Spika wa Bunge Job Ndugai.

"Namshukuru Rais wa Afrika Kusini kwani ametemblea eneo la Mazimbo mkoani Morogoro ambako kuna makaburi ya mashujaa wa Afrika Kusini.Rais wa Afrika Kusini alikutana na mabinti wawili ambao walikuwa wanamtafuta baba yao,

"Na majina yao yameonekana katika makaburi hayo.Ni uchungu sana lakini kwa sehemu kubwa inaonesha  ni namna gani Mwalimu Nyerere aliwapenda wengine," amesema Rais Magufuli.

Amefafanua kwamba wote ambao walikuwa kwenye harakati za kupigania uhuru walikuwa wanatumia lugha ya Kiswahili kwa ajili ya kuwasaliana.Hivyo ameshukuru lugha ya Kiswahili kuwa lugha ya nne rasmi ya nne kwenye jumuiya yetu.Mmemfuta machaozi baba wa Taifa.

"Kwa niaba ya Watanzania tunashukuru sana kwa lugha hii kuwa rasmi.Hivyo uamuzi huu wa kuifanya lugha hii kuwa rasmi itainganisha wananchi wetu.Kwa nchi ambazo hawazungumzi Kiswahili, Serikali ya Tanzania itakuwa tayari kutoa walimu wa somo la Kiswahili kwa ajili ya kuwafundisha wananchi wao," amesema.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...