Mkuu wa Jeshi la Polisi IGP Simon Sirro amemuagiza kamanda wa Polisi mkoa wa Tabora kuhakikisha anashirikiana na wananchi katika kudhibiti vitendo vya mauaji yanayotokana na imani za ushirikina, ubakaji pamoja na uhalifu wa uvunjaji. 

IGP Sirro amesema hayo wakati akiwa katika ziara ya ukaguzi katika wilaya za Igunga na Nzega mkoani humo ziara yenye lengo la kuona utayari wa askari Polisi wakati wanapotekeleza majukumu yao. 

Aidha, IGP Sirro amesema kuwa, ni vyema pia viongozi wa kidini na wa kisiasa kuzungumzia madhara ya mauji na uvunjaji katika maeneo yao.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...