Na Karama Kenyunko, Michuzi TV
MAMLAKA ya Usimamizi wa Shughuli za Bima nchini (TIRA) kwa
kushirikiana na Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) imeandaa mkutano wa wadau wa
bima ili utakaofanyika mkoani Mwanza mwezi huu ili kujadili maendeleo na changamoto
zinazoikabili sekta hiyo, katika kipindi cha mwaka mmoja.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam leo
Septemba 12,2019 Kamishina wa TIRA, Tanzania
Dk. Mussa Juma amesema mkutano huo amao hufanyika kila mwaka mwezi huu
wa tisa safari hii mada kubwa itakuwa ni
kuinua upenyo wa bima kwa kuongeza wigo wa bima kwa wasiokuwa na bima.
Aidha amesema mada hiyo inamalengo makuwa ya kutoa elimu ya
bima kwa jamii na jukwaa kamili kwa ajili ya wadau wa Taasisi na kuongeza
mtandao wa kibiashara kitu
kitakachoongeza malengo ya serikali ya awamu ya tano amayo imedhakia nchi
kufikia kipato cha kati ifikapo mwaka 2025.
Dk. Juma amesema, katika mkutano huo, unaotarajiwa kuanza septemba
24 hadi 29, mwaka huu, watakuwa pia watatoa elimu juu ya ufahamu wa bima,
kubadirishana maarifa na utaalamu wa bima,kutoka kwa wataalamu wa ndani na nje
ya nchi na pia katika wiki hiyo, taasisi ya bima itatoa jukwaa kamili na vifaa
muhimu kwa maendeleo, uboreshaji wa maarifa ya ima na mazoezi.
“Katika wiki hiyo tutakuwa na matemezi ya bima, Utoaji Damu
utoaji wa tunzo mbali mbali mbali za mwaka kwa washindo mbali mbali pamoja na
michezo mbali mbali kiwamo mpira wa miguu na ama mikono”, amesema Dk. Juma
Amesema pia watajadili fursa na changamoto zinazoikabili
sekta ya bima nchini pamoja na wajibu wa wasambazaji wa huduma hiyo ya bima.
"Katika mkutano huu Naibu Waziri wa Fedha na Mipango,
Dk. Ashantu Kijaji anatarajiwa kuwa mgeni rasmi, hii ni kwa sababu wizara yake
ndio yenye dhamana ya usimamizi wa sekta ya fedha na bima ikiwemo, " amesema
Dk. Juma.
Naye Katibu wa Taasisi ya Bima Tanzania, Ernest Kilumbi amesema
wiki hiyo ya bima ni jukwaa sahihi kwa ajili ya kuanzisha na kuratibu shughuli
za bima ikiwamo kutoa elimu, misaada kwa wazee, yatima na watoto wanaoishi
katika mazingira magumu.
"Wiki hii ya bima ni jukwaa kamili kabisa la
kuwakutanisha wadau kwa lengo la kupeana taarifa na kuinua upenyo na kuuongeza
kwa watu wasiokuwa na bima, " alisema.
Kwa upande wake Mwakilishi wa majaji katika utoaji tuzo za
umahiri kwenye sekta ya Bima, Frenk Kitende amesema katika mkutano huo wa TIRA
kwa kushirikiana na IIT imeona ni muhimu kuanzisha tuzo hizo ili kuweza kuwatambua
na kuzawadi ufanisi kwenye uendeshaji, uongozi na utawala wa wadau katika sekta
ya bima.
Amesema walipokea jumla ya maombi 72 ya wadau kutoka taasisi
mbali mbali za bima amapo kati ya hizo maombi 32 yalipitishwa huku 40
yakikataliwa kwa sababu mbalimbali.
"Majaji wote walifanya kazi kwa bidii kubwa kupitia
maombi ya washiriki wote na kuhakiki taarifa ziluzowasilishwa, alama za ufaulu
zitawekwa kwenye mtandao baada ya sherehe za utoaji tuzo zotakazofanyika
Septemba 26 mwaka huu, " amesema.
Kamishana wa mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima nchini (TIRA) Dk. Musa Juma akizungumza na waandishi wa habari juu ya mkutano wa wadau mbali mbali wa bima unaotarajiwa kufanyika mkoani Mwanza kuanzia Septemba 24 hadi 29,2019. Mkutano huo umeandaliwa na TIRA kwa kushirikiana na Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) kwa lengo la kujadili maendeleo na changamoto zinazoikabili tasnia ya bima katika kipindi cha mwaka mmoja.
Katibu wa Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) , Ernest Kilumbi, akizungumza katika mkutano huo
Mwakilishi wa majaji katika utoaji tuzo za umahiri katika sekta ya Bima, Frenk Kitende akielezea namna wadau mbali mbali wa tasnia ya Bima watavyopewa tuzo ya kuweza kutambua na kuzawadi ufanisi kwenye uendeshaji, uongozi na utawala wa wadau katika sekta hiyo katika mkutano huo.
Kamishana wa mamlaka ya Usimamizi wa Shughuli za Bima nchini (TIRA) Dk. Musa Juma akizungumza na waandishi wa habari juu ya mkutano wa wadau mbali mbali wa bima unaotarajiwa kufanyika mkoani Mwanza kuanzia Septemba 24 hadi 29,2019. Mkutano huo umeandaliwa na TIRA kwa kushirikiana na Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) kwa lengo la kujadili maendeleo na changamoto zinazoikabili tasnia ya bima katika kipindi cha mwaka mmoja.
Katibu wa Taasisi ya Bima Tanzania (IIT) , Ernest Kilumbi, akizungumza katika mkutano huo
Mwakilishi wa majaji katika utoaji tuzo za umahiri katika sekta ya Bima, Frenk Kitende akielezea namna wadau mbali mbali wa tasnia ya Bima watavyopewa tuzo ya kuweza kutambua na kuzawadi ufanisi kwenye uendeshaji, uongozi na utawala wa wadau katika sekta hiyo katika mkutano huo.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...