Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Angellah Kairuki akiwakabidhi taulo za kike kwa baadi ya wanafunzi wa shule ya sekondari Mkombozi iliyoko kijiji cha Hedaru wilaya ya Same mkoani Killimanjaro kama anavyoonekana katika picha.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Angellah Kairuki akizungumza na wanafunzi wa shule ya sekondari Mkombozi iliyoko kijiji cha Hedaru wilaya ya Same mkoani Killimanjaro.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Angellah Kairuki akiwakabidhi taulo za kike kwa mwalimu kwa niaba ya wanafunzi wa kike katika shule ya sekondari Mkombozi iliyoko kijiji cha Hedaru wilaya ya Same mkoani Killimanjaro kama anavyoonekana katika picha.
Na Vero Ignatus,Killimanjaro.
Waziri wa Nchi Ofisi ya Waziri Mkuu Uwekezaji Angellah Kairuki amegawa taulo za kike kwa wanafunzi wa shule ya sekondari mkombozi iliyoko kijiji cha Hedaru wilaya ya Same mkoani Killimanjaro lengo likiwa ni kuwawezesha wasichana kusoma bila usumbufu wanapokuwa katika kipindi cha hedhi.
Kairuki alifika shuleni hapo na kuzungumza na wanafunzi wa kike huku akiwataka kujiepusha na vishawishi pamoja na tamaa ili waweze kutimiza ndoto zao na kusaidia jamii inayowazunguka .
Aidha amesema kuwa ataendelea kushirikiana na shule hiyo katika kutatua changamoto mbalimbali ikiwemo ukosefu wa uzio ,uhaba wa matundu ya vyoo ili wanafnzi hao waweze kusoma katika mazingira rafiki.
Furahini Lubuwa ni wa shule ya sekondari ya mkombozi,hiyo amempongeza Waziri Kairuki kwa kutembelea wanafunzi hao na kuwapatia msaada wa taulo za kike kwani zitawasaidia hasa wale ambao wanatoka katika familia zenye kipato cha chini .
Fatuma Hemed ni mmoja wa Wanafunzi wa Shule hiyo amesema kuwa msaada huo utawawezesha kusoma bila usumbufu kwani wapofikia kipindi cha hedhi huwa na hofu hasa wale ambao hawawezi kujisitiri vyem hivyo msaada huo utawasaidia.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...