Mkurugenzi Mtendaji wa Bodi ya Utalii Tanzania, Bi. Devotha Mdachi akiwakaribisha watalii kutoka nchini Israel mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro kwa ndege ya shirika la El Al Israel, leo tarehe 12 Oktoba 2019.Watalii wapatao 920 wameendelea kuwasili nchini katika makundi tofauti ambapo Watalii wanaowasili kupitia uwanja wa Kimataifa wa Kilimanjaro wanatarajiwa kufika 720 na Watalii 200 kwa wale waliokwishawasili kupitia Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Abeid Amani Karume, Zanzibar. 
Sehemu ya Watalii kutoka nchini Israel wakipata huduma mara baada ya kuwasili ndani ya Uwanja wa ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro.Wakiwa nchini watalii hao watatembelea hifadhi ya Serengeti, Ngorongoro, Tarangire, Manyara pamoja na Zanzibar ili kuweza kujionea vivutio mbalimbali na kujifunza mambo mbalimbali ya mila na utamaduni wa kitanzania. 
Sehemu nyingine ya Watalii kutoka nchini Israel wakipata huduma mara baada ya kuwasili katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro. 
Kikundi cha ngoma cha Wamasai kikitumbuiza katika Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Kilimanjaro ikiwa ni ishara ya kuwalaki wageni hao. 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...