Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP - Phaustine Kasike akisalimiana na
Meneja Miradi wa Asasi ya Kidini ya New Life In Christ Mkoani Kilimanjaro, Bw. Charles
Shang’a alipowasili katika viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi kwa ajili ya hafla fupi ya
kupokea Misaada ya Kibinadamu iliyotolewa na Asasi hiyo kwa ajili ya wafungwa leo
Novemba 15, 2019.
Meza kuu wakiongozwa na Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP - Phaustine
Kasike (wa pili toka kushoto) wakiimba wimbo wa Taifa la Tanzania ikiashiria ufunguzi wa
hafla fupi ya kupokea misaada ya Kibinadamu kwa ajili ya wafungwa iliyotolewa na Asasi
ya Kidini ya New Life In Christ. Tukio hilo limefanyika leo Novemba 15, 2019 katika
viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi.
Kaimu Mkurugenzi wa Asasi ya Dorcas Aid International Tanzania Bw. Joseph
Kumwembe akitoa maelezo mafupi kabla ya kukabidhi msaada wa Kibinadamu kwa ajili ya
Wafungwa nchini. Dorcas Aid International Tanzania hushirikiana na Asasi ya Kidini ya
New Life In Christ katika kutoa misaada ya namna hiyo.
Kamishna Jenerali wa Magerezanchini, CGP - Phaustine Kasike akitoa hotuba kwa
wageni mbalimbali (hawapo pichani) waliohudhuria hafla fupi ya kupokea msaada wa
Kibinadamu kwa ajili ya wafungwa kutoka kwa Asasi ya Kidini ya New Life In Christ leo
Novemba 15, 2019 katika viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, CGP - Phaustine Kasike akipokea msaada
wa baiskeri ya walevu pamoja na vitu mbalimbali vilivyotolewa na Asasi ya Kidini ya New
Life In Christ leo Novemba 15, 2019 kwa ajili ya wafungwa. Hafla ya upokeaji wa misaada
hiyo imefanyika katika gereza Kuu Karanga Moshi.
Muonekano wa baadhi ya misaada ya Kibinadamu iliyotolewa Asasi ya Kidini ya
New Life In Christ iliyokabidhiwa kwa Jeshi la Magereza leo Novemba 15, 2019 katika
viwanja vya Gereza Kuu Karanga Moshi. Misaada imekabidhiwa leo kwa ujumla wake ina
thamani ya zaidi ya milioni 183.
Mhandisi ujenzi wa Jeshi la Magereza, SP. Julius Sukambi akitoa maelezo ya
kitaalam kwa Kamishna Jenerali wa Magerezanchini, CGP - Phaustine Kasike alipotembelea
katika eneo hilo la ujenzi wa Kiwanda Kipya cha bidhaa za ngozi kinachojengwa nje ya eneo
la Gereza Kuu Karanga, Moshi(Picha zote na Jeshi la Magereza).
Na ASP Lucas Mboje, Moshi
ASASI ya Kidini ya New Life In Christ imekabidhi kwa Jeshi la Magereza misaada ya vitu
mbalimbali yenye thamani ya zaidi ya shilingi milioni 183 ambayo itawanufaisha wafungwa
na Mahabusu waliopo magerezani katika Mikoa ya Arusha, Kilimanjaro na Tanga.
Akizungumza kabla ya kukabidhi misaada hiyo ya wahalifu waliopo magerezani, Kaimu
Mkurugenzi wa Asasi ya Dorcas Aid International Tanzania, Bw. Joseph Kumwembe
amesema vifaa vilivyokabidhiwa ni magodoro, sabuni, nguo za watoto, mabranketi,
vipeperushi, vifaa vya usafi na vitabu vya kiroho.
Kwa upande wake, Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike ameishukru
Asasi hiyo isiyo ya Kiserikali kwa kuendelea kuunga mkono juhudi za Serikali katika
kutekeleza kwa ukamilifu utoaji wa misaada ya kibinadamu pamoja na baadhi ya huduma
muhimu kwa wafungwa ikiwemo mafunzo ya Kijasiriamali kwa wafungwa hivyo kulisaidia
Jeshi la Magereza katika suala zima la urekebishaji wa wafungwa.
“Niwashukru sana Asasi hii kwa moyo wao wa upendo na kujitolea na niwapongeze sana
kwa kutambua kwamba wahalifu waliopo magerezani ni Binadamu kama walivyo Binadamu
wengine na wanahitaji misaada ya ki-binadamu kama hii,” Amesema Jenerali Kasike.
Aidha, Jenerali Kasike ametoa wito kwa Asasi nyingine zisizo za Kiserikali kuiga mfano
uliooneshwa na New Life in Christ na Dorcas Aid International Tanzania ili ziweze
kushirikiana na Jeshi la Magereza kwa manufaa ya Taifa.
Katika hatua nyingine, Kamishna Jenerali Kasike amewataka Wakuu wote wa Magereza
yaliyonufaika na misaada hiyo kuhakisha kuwa misaada inawanufaisha walengwa kwa
maeneo yaliyokusudiwa samabamba na kusimamia vyema vifaa hivyo.
Kamishna Jenerali wa Magereza nchini, Phaustine Kasike mara baada ya kupokea misaada
hiyo ametembelea eneo la mradi mkubwa wa uwekezaji wa Kiwanda kipya cha bidhaa za
ngozi ambacho ni cha ubia kati ya Jeshi la Magereza pamoja na Mfuko wa hifadhi ya jamii
wa PSSSF. Kiwanda hicho kinajengwa katika eneo lililopo nje ya Gereza Kuu Karanga,
Moshi ambapo amewasisitiza wakandarasi wa ujenzi huo kufanya kazi usiku na mchana ili
kukamilisha mradi huo kwa wakati.
Toa Maoni Yako:
0 comments so far,add yours
Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...