Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu anayeshughulikia Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akizungumza na viongozi wa Chama cha Waajiri (ATE) na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) walipokutana kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya Wafanyakazi na Waajiri, Novemba 2, 2019 Jijini Dodoma.
Sehemu ya viongozi wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi nchini (TUCTA) wakifuatilia maelezo ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama (hayupo pichani) alipokutana nao Bungeni, Jijini Dodoma. Kushoto ni Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya.
Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe akifafanua jambo wakati wa kikao hicho cha Utatu kilichowakutanisha kwa ajili ya kujadili masuala mbalimbali ya Wafanyakazi na Waajiri.

Baadhi ya wajumbe kutoka Chama cha Waajiri (ATE) na Ofisi ya Waziri Mkuu wakifuatilia majadiliano wakati wa mkutano huo uliofanyika Jijini Dodoma.
Rais wa Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) Bw. Tumaini Nyamhokya akieleza jambo wakati wa mkutano huo.
Waziri wa Nchi, Ofisi ya Waziri Mkuu Sera, Bunge, Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Mhe. Jenista Mhagama akipitia taarifa wakati wa mkutano na viongozi wa Chama cha Waajiri (ATE) na Shirikisho la Vyama vya Wafanyakazi (TUCTA) walipokutana kwa lengo la kujadili masuala mbalimbali ya Wafanyakazi na Waajiri, Jijini Dodoma.
Mkuu wa Huduma za Kisheria kutoka Chama cha Waajiri (ATE) Bi. Suzan Ndomba akichangia mada wakati wa mkutano huo uliofanyika Jijini Dodoma. Kulia ni Katibu Mkuu, Ofisi ya Waziri Mkuu Kazi, Vijana, Ajira na Wenye Ulemavu Bw. Andrew Massawe.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...