Kampuni ya simu za mkononi ya Airtel leo imetangaza na kuzindua kampeni maalum ambayo inayojulikana kama LIPA ADA kwa Airtel Money itakayotoa  suluhisho kwa  wateja wake kuweza kufanya malipo yoyote ya karo za shule ambapo kwa sasa wateja wataweza kulipa karo kwa kutumia akaunti zao za Airtel Money wakiwa popote katika  kipindi hiki cha msimu wa sikukuu na kuendelea.
Akizungumza leo jijini Dar es Salaam wakati wa kutangaza kampeni hiyo, Mkurugenzi wa Airtel Money Isack Nchunda alisema kuwa LIPA ADA kwa kutumia Airtel Money itakuwa ni suluhisho kwa wazazi wengi ambao wamekuwa wakipoteza muda mwingi wa kwenda kupanga foleni benki ili kulipia watoto wao karo na vile vile itaendela kutoa hamasa kwa wateja wa Airtel kuendelea kutumia Airtel Money kulipia malipo mbali mbali ya bidhaa na huduma.
‘Kama mnavyojua, hiki ni kipindi cha wazazi na familia kuwa katika mapumziko, lakini pia muda huu wazazi huutumia kulipia karo za shule za watoto wao. Natoa wito kwa Watanzania kuendelea kutumia Airtel Money kwa malipo yao kwani ni njia rahisi, haraka na nafuu kwa malipo wakiwa popote wanaweza kulipa sio lazima kwenda bank na kupanga foleni, Nchunda alisema.
Nchunda alisema kuwa Airtel imeamua kuja na kampeni ya LIPA ADA kwa Airtel Money kama njia mojawapo ya kutoa suluhisho ya kifedha kwa Watanzania. ‘Kama mnavyojua, kulingana na utafiti wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA) wa hivi karibuni kuonyesha kuwa zaidi ya Watanzania milioni 22.9 wanatumia huduma za kifedha kwa kutumia simu zao huku miamala yenye dhamani ya zaidi ya Trilioni 8 ikifanyika mpaka kufikia Juni 2019. Kwa miaka ya hivi karibuni, huduma za kifedha kwa simu za mkononi imebadilika kutoka huduma ya kawaida kama vile kununua muda wa maongezi mpaka kuwa moja ya huduma muhimu inayowezesha ukuaji sekta na  mzunguko wa fedha kila mahali.
Jinsi ya kulipia Ada Kwa Airtel Money:
  • Piga *150*60# Ili kufikia Kwenye Menyu ya Airtel Money
  • Chagua 5: Lipia Bili
  • Chagua 4: Weka namba ya kampuni (Namba ya Malipo ya Shule)
  • Ingiza Kiasi cha pesa
  • Ingiza Namba ya Kumbukumbu (Jina la mwanafunzi na Kidato / Namba ya kitambulisho cha mwanafunzi )
  • Ingiza Namba ya siri
Kwa upande wake, Mkurugenzi wa Mawasiliano Airtel Tanzania Beatrice Singano alisema kuwa Airtel inajivunia kuwa kampuni ya simu za mkononi ambayo sasa inakuza kwa kasi mtandao wa huduma za kifedha hapa nchini.

“Airtel tumejipanga na kujikita katika mipango yetu ya kuendelea kupanua wingo wa huduma zetu, Airtel kwa sasa tuna maduka ya Airtel Money branches Zaidi ya 1000 nchi nzima ikiwa ni moaja kati ya mpango yetu ya kuleta suluhisho za kifedha pamoja na kusambaza huduma na bidhaa zetu karibu na wateja. Dhamira yetu ni kuendelea kujenga mtandao imara na unaotegemewa’. Alisema Singano huku akiongeza kuwa huduma na bidhaa za Airtel kama vile kurundisha muamala uliokosewa, kubadilisha PIN, kusajili laini za simu kwa kutumia alama ya vidole zinapatikana kwenye maduka yote ya Airtel Money branches.
 Mkurugenzi wa Airtel Money, Isack Nchunda  akizungumza wakati wa kuzindua kampeni maalum inayojulikana kama LIPA ADA kwa Airtel Money itakayotoa suluhisho  kwa wateja wa Airtel Money kuweza kufanya malipo yoyote ya karo za shule  kwa kutumia akaunti zao za Aitel Money wakiwa popote katika kipindi hiki cha msimu wa Sikukuu na kuendelea Kushoto ni Meneja wa Airtel Jackson Mmbando



Meneja wa Airtel Jackson Mmbando akifafanua jambo wakati wa kuzindua kampeni maalum inayojulikana kama LIPA ADA kwa Airtel Money itakayowawezesha  kwa wateja Airtel kuweza kufanya malipo yoyote ya karo za shule kupitia akaunti zao za Aitel Money wakiwa popote wakati msimu huu wa Sikukuu na kuendelea, hafla ya uzinduzi ilifanyika ofisi kuu ya Airtel  jijini Dar es Salaam jana.Katikati ni Mkurugenzi wa Airtel Money, Isack Nchunda na kulia ni Mkuu wa Kitengo cha lipa Ada kwa Airtel Money. Emmanuel Mwaisoloka

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...