NA MWAMVUA MWINYI,KIBAHA 

MKUU wa wilaya ya Kibaha ,mkoani Pwani ,Assumpter Mshama ameeleza iko haja ya kuwa na usawa wa kijinsia kwa watoto wa kike na wa kiume pindi mwanafunzi wa kike anapopata mimba akiwa shuleni,ili iwe fundisho kwa wanafunzi wengine . 

Ameeleza, inapaswa mtoto wa kike nae achukuliwe hatua sawa na mtoto wa kiume kwani ujauzito hautokani na upande mmoja bali ni ushirika wa watu wawili wa jinsia mbili tofauti. 

Akizungumza katika mahafali ya wanafunzi wa chuo cha ufundi stadi VETA Pwani , pamoja na mambo mengine, Mshama anasema ifikie hatua kila mwanafunzi apate adhabu sawa baada ya kupeana mimba ili kukomesha tabia hiyo. 

“Kwa wilaya hii wote mtapata adhabu, haiwezekani mtoto wa kike aendelee kutamba wakati muda mwingine unakuta mtoto huyo ndio alikuwa chanzo cha kumtongoza mwalimu au mwanafunzi mwenzie,hamjawahi kuona hilo

Aidha Mshama alishauri Vijana hao waliomaliza chuo cha ufundi stadi VETA, kujiajiri kwa kufungua viwanda vidogo vidogo na kutengeneza vifaa vyenye ubora ili waweze kupambana na tatizo la ukosefu wa ajira. 

Mapema wakisoma risala yao mbele ya mgeni rasmi wanachuo ZAHARA ABDUL na IDD ATHUMANI waliiomba serikali ya mkoa huo,kutoa kipaumbele cha ajira na fursa mbalimbali zilizoko ndani ya mkoa.
Nae kaimu mkuu wa chuo hicho ,Karim aliainisha changamoto kubwa inayoikabili chuo ni upungufu wa mabweni.
 

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...