Allen Christian na Collin Ndanzi (DSJ)

MAHAKAMA  ya Hakimu Mkazi kisutu imeuambia upande wa utetezi katika kesi ya uhujumu uchumi inayomkabili Mwandishi wa habari za uchunguzi Erick Kabendera kuwa waende wenyewe kwa mkurugenzi wa mashtàka nchini (DPP) ili kujua hatma ya barua ya mshtakiwa ya makubaliano ya kuomba msamaha na kukiri kosa ( pre- baggening).

Hatua hiyo imefikiwa wakati kesi hiyo leo Desemba 4, 2019 ilipoitwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Janet Mtega  kwa ajili ya kutajwa na kudaiwa kuwa upelelezi bado haujakamilika hivyo upande wa utetezi wakawasilisha hoja zao.

Mapema wakili wa utetezi Jebra Kambole alidai mahakamani hapo kuwa, Oktoba 11, 2019 waliitaarifu mahakama juu mshtakiwa kuandika barua ya kuomba msahama na kukiri kosa kwenda kwa DPP lakini mpaka leo ni miezi miwili hawajapata mrejesho wowote kutoka kwa DPP .

"Ni lini tutakamilisha mchakato wa majadiliano hayo kwani mpaka sasa hakuna chochote ambacho kimefanyika na mtuhumiwa bado yuko gerezani na ni mgonjwa", ameuliza Kambole

Akijibu hoja hizo wakili wa serikali Easter Martin amekiri kwamba ni kweli maombi yao hayo yapo kwa DPP toka Oktoba 11 hadi leo lakini suala la makubaliano si maamuzi yanayoweza kutolewa mara moja,  ni vema waende katika ofisi ya DPP ili wajue kinachoendela.

Hakimu Mtega nae amesema, kufuatia hoja hizo,  amewataka upande wa utetezi waende wenyewe kufuatilia jalada la kesi kwa DPP ili wajue kinachoendelea na ameiahirisha kesi hiyo hadi itakapotajwa tena Desemba 18, mwaka huu.

Katika kesi hiyo, Kabendera anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka matatu likiwemo la utakatishaji wa Sh milioni 173.

Katika mashtaka ya kwanza ilidaiwa kuwa katika kipindi hicho, Kabendera alijihusisha  na mtandao wa kihalifu kwa kutoa msaada kwa genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia faida.

Inadaiwa kuwa katika kipindi hicho,bila ya sababu,alikwepa kodi ya Sh 173,247,047.02 ambayo ilitakiwa ilipwe Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Pia inadaiwa Kabendera alitakatisha Sh 173,247047.02 huku akijua fedha hizo ni mazalia ya kosa la kujihusisha na genge la uhalifu na ukwepaji kodi.

Mwimsamaha na kukiri kosa ( pre- baggening).

Hatua hiyo imefikiwa wakati kesi hiyo leo Desemba 4,2019 ilipoitwa mahakamani hapo mbele ya Hakimu Mkazi Mkuu, Janet Mtega  kwa ajili ya kutajwa na kudaiwa kuwa upelelezi bado haujakamilika hivyo upande wa utetezi wakawasilisha hoja zao.

Mapema wakili wa utetezi Jebra Kambole alidai mahakamani hapo kuwa, Oktoba 11,2019 waliitaarifu mahakama juu mshtakiwa kuandika barua ya kuomba msahama na kukiri kosa kwenda kwa DPP lakini mpaka leo ni miezi miwili hawajapata mrejesho wowote kutoka kwa DPP .

"Ni lini tutakamilisha mchakato wa majadiliano hayo kwani mpaka sasa hakuna chochote ambacho kimefanyika na mtuhumiwa bado yuko gerezani na ni mgonjwa", ameuliza Kambole

Akijibu hoja hizo wakili wa serikali Easter Martin amekiri kwamba ni kweli maombi yao hayo yapo kwa DPP toka Oktoba 11 hadi leo lakini suala la makubaliano si maamuzi yanayoweza kutolewa mara moja,  ni vema waende katika ofisi ya DPP ili wajue kinachoendela.

Hakimu Mtega nae amesema, kufuatia hoja hizo,  amewataka upande wa utetezi waende wenyewe kufuatilia jalada la kesi kwa DPP ili wajue kinachoendelea na ameiahirisha kesi hiyo hadi itakapotajwa tena Desemba 18, mwaka huu.

Katika kesi hiyo, Kabendera anakabiliwa na kesi ya uhujumu uchumi yenye mashtaka matatu likiwemo la utakatishaji wa Sh milioni 173.

Katika mashtaka ya kwanza ilidaiwa kuwa katika kipindi hicho, Kabendera alijihusisha  na mtandao wa kihalifu kwa kutoa msaada kwa genge la uhalifu kwa nia ya kujipatia faida.

Inadaiwa kuwa katika kipindi hicho,bila ya sababu,alikwepa kodi ya Sh 173,247,047.02 ambayo ilitakiwa ilipwe Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA).

Pia inadaiwa Kabendera alitakatisha Sh 173,247047.02 huku akijua fedha hizo ni mazalia ya kosa la kujihusisha na genge la uhalifu na ukwepaji kodi.

Michuzi Blog

Tanzanian blog operating since 2005, covering International news and Local News, including Politics, Fashion, Social Scenes, Interviews, Movies, Events, personalities and anything positive happening worldwide. Written in Swahili and English targeting both Swahili and English readers.

Toa Maoni Yako:

0 comments so far,add yours

Hii ni Blog ya Watanzania popote walipo duniani kwa ajili ya kuhabarisha, kutoa/kupokea taarifa na kuelimisha mambo yote yaliyo chanya kwa Taifa letu. Tafadhali sana unapotoa maoni usichafue hali ya hewa wala usijeruhi hisia za mtu/watu. Kuwa mstaarabu...